Page 99 - Historia_Maadili
P. 99

Mapinduzi ya Zanzibar yalitokana na sababu nyingi za kijamii, kiuchumi na kisiasa.
          Kwa mfano, Waarabu, ambao walikuwa wachache, walipewa upendeleo na walitawala

          kisiasa na kiuchumi. Hali hii  haikuwaridhisha Waafrika waliokuwa wengi. Waarabu
          walihodhi madaraka, ardhi na utajiri mwingine wa Zanzibar, huku Waafrika wakiwa
          wafanyakazi wa watawala.
        FOR ONLINE READING ONLY

          Aidha, jamii ya Zanzibar iliathiriwa kwa kiasi kikubwa na mchanganyiko mkubwa
          wa watu wenye tamaduni tofauti. Kulikuwa na watu wenye tamaduni za Waarabu,
          Waafrika na Wahindi. Hivyo, jamii iligawanyika katika makundi ya watu kulingana

          na rangi na asili ya jamii iliyohusika. Kwa mfano, jumuiya za Waarabu, hususani
          Waarabu wa Oman, walikuwa na nguvu kubwa za kisiasa na kiuchumi na walikuwa na

          hadhi ya  juu zaidi. Wahindi walikuwa na nguvu za kiuchumi kwa kushikilia biashara
          nyingi, hivyo  walikuwa ni kundi lenye hadhi ya kati. Wakati huo huo, Waafrika
          waliokuwa wengi  na walikuwa na hadhi ya  chini kabisa katika jamii, wakiwa

          hawana nguvu za utawala wala uchumi. Utaratibu huu uliathiri kanuni za kimaadili
          na kijamii za wakati huo, kwani heshima, utu na tabia ziliamuliwa kutokana na asili

          (rangi), hadhi na nafasi ya mtu katika jamii.

          Kutokana na kukosa haki zao za msingi, vyama vya siasa vya ASP, ZNP na ZPPP
          viliongeza shinikizo kwa serikali ya kikoloni kuwapatia uhuru Wazanzibari. Vuguvugu

          hili halikuwa rahisi na lilichukua sura na mitazamo tofauti. Hata hivyo, baada ya
          malumbano makali na chaguzi nyingi kufanyika, Uingereza iliutoa uhuru kwa Zanzibar
          tarehe 10 Desemba 1963. Uhuru huu ulikuwa wa serikali ya mseto wa vyama vya

          ZNP na ZPPP. Katika kipindi hiki, Waziri Mkuu alikuwa Mohammed Shamte, huku
          Sultani Jamshid bin Abdullah Al Said akibaki kwenye nafasi yake kama kiongozi wa

          nchi. Uhuru huu haukuungwa mkono na wengi, hasa Waafrika, ambao waliona kuwa
          Waingereza wamekabidhi serikali kwa Waarabu badala ya wananchi wote.

          Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalikuwa ni kilele cha harakati za mapambano

          ya ukombozi wa Wazanzibari. Mapambano haya yalikuwa ni matokeo ya uchaguzi
          na uhuru uliotolewa tarehe 10 Desemba 1963 chini ya serikali ya Waziri Mkuu
          Mohammed Shamte na Sultani Jamshid bin  Abdullah  Al Said, uhuru ambao

          ulijulikana kama “uhuru wa wachache.” Hivyo, kufikia tarehe 12 Januari 1964,





                                                  91




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   91
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   91                                         03/10/2024   18:15:19
   94   95   96   97   98   99   100   101   102   103   104