Page 104 - Historia_Maadili
P. 104

Zoezi la          6.3


            1.  Eleza nafasi ya ASP katika kufanikisha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

            2.  Eleza ni kwa namna gani huduma za kijamii kama vile elimu, afya na makazi
        FOR ONLINE READING ONLY
               zilitolewa   kulingana na matabaka ya rangi Zanzibar.

            3.  Ni kwa namna gani ubaguzi wa rangi ulichochea Mapinduzi Matukufu ya
               Zanzibar?








           Kazi ya kufanya 6.2


            Soma matini mbalimbali kupitia mtandao yanayohusu Mapinduzi Matukufu ya
            Zanzibar, kisha andika maelezo kwa ufupi kuhusu:
             (a)  Namna Mapinduzi yalivyofanyika;

             (b)  Viongozi walioongoza Mapinduzi; na
             (c)  Ulichojifunza kutokana na Mapinduzi hayo.




          Mchango wa Mapinduzi wa Matukufu ya Zanzibar

          Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964 yalileta mabadiliko makubwa
          katika historia ya Zanzibar na yalikuwa na athari kubwa katika ukanda wa Afrika
          Mashariki na maeneo mengine. Mapinduzi hayo yalisababisha kuondolewa kwa
          utawala wa kisultani na kuanzishwa kwa serikali iliyoongozwa na wazalendo wa
          Chama cha Afro-Shirazi (ASP). Chama cha ASP kiliongoza kwa misingi ya utu, haki
          na ustawi wa watu wote bila kuzingatia tofauti za asili, hadhi au kabila. Mchango
          wa Mapinduzi hayo unajidhihirisha katika nyanja mbalimbali kama vile kujenga
          umoja, kuimarisha mshikamano na kuendeleza maadili katika jamii za Kizanzibari
          na Tanzania kwa ujumla.


          Kujenga umoja

          Mapinduzi yalisaidia kuvunja migawanyiko na chuki zilizojengwa kutokana na hali
          ya ubaguzi katika jamii wakati wa ukoloni. Kwa kuwapindua watawala waliokuwa
          wakionekana kama wawakilishi wa wakoloni walioondoka, Mapinduzi yalileta umoja


                                                  96




                                                                                        03/10/2024   18:15:20
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   96
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   96                                         03/10/2024   18:15:20
   99   100   101   102   103   104   105   106   107   108   109