Page 102 - Historia_Maadili
P. 102

Mathalani, uchaguzi wa Julai 1963 uliwapa ushindi muungano wa ZNP na ZPPP
          ambao walipata viti 18 dhidi ya viti 13 vya ASP. Mohamed Shamte wa ZPPP akawa
          Waziri Mkuu wa kwanza wa Zanzibar, jambo ambalo lilionekana kuwa ni la upendeleo
          na kuuendeleza ubaguzi. Wazanzibari walichoka kutawaliwa na wageni kwa muda
          mrefu na walihitaji kujitawala wenyewe. Hivyo basi, Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
          yalikuwa ni hatua muhimu ya kujikomboa na kuupata uhuru ili kujenga maendeleo,
        FOR ONLINE READING ONLY
          kulinda utamaduni na maadili ya watu wa Zanzibar.

          Sababu za kijamii: Kabla ya kuja kwa utawala wa Waarabu, utamaduni wa jadi wa
          jamii za Kizanzibari ulikuwa na tabia na sifa maalumu zinazotokana na mazingira,
          mila na desturi za jamii hizo. Wazanzibari walifundishwa kuheshimu watu wa rika
          zote, wakiwemo wazazi, wazee na viongozi wa mila. Aidha, watoto walilelewa kwa
          kushiriki katika kazi za kijamii kama kilimo na uvuvi. Pia, kulikuwa na mgawanyo
          wa majukumu katika familia na jamii. Kwa mfano, wanawake walijihusisha na
          shughuli za ususi wa vikapu na mikeka kwa kutumia majani mbalimbali kama ya
          ukindu, minazi na miti ya porini.  Wanaume walijihusisha na uvuvi, uwindaji, kilimo,
          pamoja na ufundi wa kutengeneza zana za kilimo na uvuvi. Pia wanaume walijenga
          nyumba za jadi kwa kutumia udongo, makuti, mawe na miti hasa mikoko.

          Vilevile, jamii iliishi kwa kuzingatia misingi ya umoja, haki na amani. Matukio kama
          vile harusi, tohara na mazishi yalitumika kuwaunganisha watu pamoja. Vyombo vya
          muziki kama ngoma, njuga, filimbi na marimba vilikuwa maarufu katika kuenzi
          maadili na utamaduni wa Wazanzibari. Muziki na ngoma za jadi zilitumika katika
          sherehe na matukio haya muhimu ya kijamii kama vile unyago kwa wasichana na
          jando kwa wavulana. Hivyo, maadili haya na utamaduni wa jadi vilijenga msingi wa
          jamii ya Wazanzibari kabla ya kuja kwa wageni ambao walileta athari za kiutamaduni,
          kisiasa, kiuchumi na kijamii.

          Kuja kwa ukoloni kulileta ubaguzi katika jamii. Watu walianza kuheshimiwa kutokana
          na vyeo na asili yao (rangi). Maadili ya kuheshimu watu wa rika na tabaka zote
          hayakuzingatiwa. Vilevile, huduma za jamii kama vile maji, umeme na makazi
          zilitolewa kwa ubaguzi. Wazanzibari walibaguliwa katika nyanja za elimu, afya,
          makazi na umiliki wa rasilimali kama vile ardhi. Kwa mfano, mwaka 1955, asilimia
          14 ya bajeti ya Serikali katika  elimu ilielekezwa kwenye  shule za Wahindi, wakati
          kipindi hicho  Wahindi walikuwa 6%  tu ya watu wote wa Zanzibar. Huduma muhimu
          za kijamii, kama vile maji safi, umeme na makazi, ziliimarishwa katika Mji Mkongwe
          ambako tabaka la Waarabu, Wahindi, pamoja na familia za wakoloni au Wazungu
          ziliishi. Huduma hizi hazikupatikana maeneo mengine kama Ng’ambo ambako
          Waafrika wengi waliishi.





                                                  94




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   94                                         03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   94
   97   98   99   100   101   102   103   104   105   106   107