Page 101 - Historia_Maadili
P. 101

12 Januari 1964, Mapinduzi Matukufu ya
          Zanzibar yalifanyika. Sultani Jamshid bin
          Abdullah Al Said aling’olewa madarakani
          pamoja na serikali yake chini ya Waziri
          Mkuu Mohamed Shamte wa ZPPP.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Hatimaye tarehe 12 Januari 1964, Serikali
          ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya ASP
          ikatangazwa. Kielelezo 6.2 kinaonesha
          baadhi ya viongozi walioshiriki katika
          Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.     Kielelezo 6.2: Baadhi ya viongozi walioshiriki
                                                   Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar mwaka 1964

          Kulikuwa na sababu kadhaa zilizosababisha Mapinduzi ya Zanzibar. Sababu hizi
          zilichochewa na madai ya muda mrefu dhidi ya utawala wa sultani, ambaye alionekana
          kuwa mwakilishi wa Waingereza. Baadhi ya sababu hizo ni kama zifuatazo:

          Sababu za kisiasa: Kabla ya ujio wa Waarabu, Zanzibar ilikuwa imegawanyika
          katika maeneo mbalimbali ya kiutawala na kila eneo lilikuwa na kiongozi wake.
          Baadaye, watawala wa kienyeji kama vile Mwinyi Mkuu kwa upande wa Unguja
          na Makamandume kwa Pemba, waliunganisha mamlaka ndogondogo na kuunda
          himaya kubwa zaidi. Viongozi hawa walizisimamia sheria na taratibu za kijamii na
          waliheshimiwa sana. Walikuwa na jukumu la kuamua migogoro, kuongoza sherehe za
          kijamii na kusimamia maadili katika jamii walizoziongoza. Hata hivyo, hali ilibadilika
          baada ya kuja kwa utawala wa wageni, hasa kuanzia kipindi cha Usultani wa Waarabu.
          Watawala wa kienyeji waliondolewa na katika utawala huu, kuanzia wakati wa
          usultani hadi ukoloni wa Waingereza, masilahi ya wenyeji hayakuzingatiwa wala
          hayakupewa kipaumbele. Kwa mfano, wenyeji hawakushirikishwa kwenye vyombo
          vya kutoa uamuzi na kuwa viongozi serikalini.

          Hata hivyo, kulikuwa na mabadiliko kidogo baada ya kuundwa kwa Baraza la Kutunga
          Sheria mwaka 1925. Wakati huu Waafrika wachache walipata nafasi, ingawa idadi
          kubwa ya wajumbe ilikuwa ni Waarabu na Wahindi. Wazanzibari hawakupata uhuru wa
          kujitawala na kufanya uamuzi wao wenyewe. Wajumbe hawa wachache hawakuweza
          kutetea masilahi ya Waafrika walio wengi Zanzibar. Hata uhuru uliopatikana baada
          ya uchaguzi wa mwaka 1963 ulikuwa ni mwendelezo wa mizizi ya ukoloni ya
          kutowatendea haki na heshima Wazanzibari.

          Vilevile, chaguzi zote tatu zilitawaliwa na mizengwe iliyosababisha kukataliwa kwa
          matokeo. Chaguzi zilifuatiwa na fujo na ulaghai na ushindi wa ASP haukutambuliwa.




                                                  93




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   93                                         03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   93
   96   97   98   99   100   101   102   103   104   105   106