Page 100 - Historia_Maadili
P. 100

yalifanyika mapinduzi rasmi Zanzibar chini
          ya uongozi wa mwanamapinduzi Sheikh Abeid

          Amani Karume, ambaye aliiongoza Zanzibar
          kuanzia mwaka 1964 hadi alipouawa tarehe 7
          April1972. Kielelezo 6.1 kinaonesha aliyekuwa
        FOR ONLINE READING ONLY
          Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya
          Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar
          na  Mwenyekiti  wa  Baraza  la  Mapinduzi,

          Sheikh Abeid Amani Karume.                      Kielelezo 6.1: Sheikh Abeid Amani
                                                                     Karume

                              Zoezi la          6.2




            1.  Fafanua sababu za kihistoria zilizosababisha  Mapinduzi Matukufu ya
               Zanzibar mwaka 1964.
            2.  Eleza  mchango  wa  Sheikh  Abeid  Aman Karume kwenye Mapinduzi
               Matukufu ya Zanzibar.

            3.  Eleza  mchango  wa vijana  katika  kufanikisha  Mapinduzi  Matukufu ya
               Zanzibar.





          Sababu za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar

          Kama ilivyoelezwa hapo awali, Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalikuwa matokeo
          ya upendeleo uliokuwepo tangu enzi za ukoloni, upendeleo ambao ulisababisha
          ubaguzi mkubwa katika sekta mbalimbali na kuwafanya Waafrika kuwa duni na
          wanyonge. Ubaguzi huu ulikuwa pigo kubwa kwa Waafrika kisiasa, kiuchumi na
          kijamii. Hali hii iliwapa Waafrika msukumo na hamasa ya kupigania haki na usawa

          katika nyanja za siasa, uchumi na utamaduni.

          Wakati wa harakati za ukombozi wa Zanzibar, mfumo wa kimaadili ulikuwa
          umeathiriwa sana na mazingira ya kiuchumi, kijamii na kisiasa. Tabaka la Waafrika
          lilikuwa limebaguliwa na wakoloni kwa muda mrefu katika nyanja zote. Hivyo, Kamati
          ya vijana jasiri na shupavu iliundwa mapema hata kabla ya uhuru wa bandia wa tarehe
          10 Desemba 1963. Lengo la kamati hiyo lilikuwa ni kuratibu kwa usiri wa hali ya juu
          suala zima la mapinduzi. Vijana hawa walifanya maandalizi yote na mnamo tarehe



                                                  92




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   92                                         03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   92
   95   96   97   98   99   100   101   102   103   104   105