Page 95 - Historia_Maadili
P. 95

Kuibuka kwa tabaka la mabepari uchwara: Kama ilivyokuwa katika nchi nyingine
          nyingi za Afrika, tabaka jipya la mabepari uchwara waliokuwa wamechukua madaraka
          serikalini walianza kutumia nyadhifa zao kujinufaisha. Wananchi walianza kushuhudia
          viongozi wakiishi maisha ya anasa  huku raia wa kawaida wakibaki masikini. Hali
          hii ilikuwa tishio kwa umoja, maadili, amani na mshikamano uliokuwa unasisitizwa
          na kujengwa mara baada ya uhuru.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Hali mbaya ya uchumi: Katika kipindi hiki, hali mbaya ya uchumi ilitokea na kuathiri
          sana upatikanaji wa huduma za kijamii kama elimu, afya na nyinginezo zinazotolewa
          na serikali. Tatizo hili lilisababisha pia ukosefu wa wataalamu, teknolojia duni,
          kuongezeka kwa maradhi, ujinga na umaskini, pamoja na kuwapo kwa miundombinu
          mibovu. Uchumi ulitegemea kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa malighafi badala ya
          bidhaa za viwandani. Hata hivyo, serikali ilianza kuchukua hatua za mageuzi ili
          kurekebisha changamoto hizi.

          Serikali pia ilikabiliwa na changamoto za kifedha na kiutawala katika kutoa huduma
          za afya kwa umma. Juhudi za kuanzisha zahanati na hospitali mpya zilikwamishwa na
          upungufu wa vifaa na wahudumu wa afya wenye sifa. Hali hii ilisababisha huduma za
          afya kutokidhi mahitaji katika baadhi ya maeneo. Pia, utegemezi wa misaada kutoka
          mataifa mengine ulifanya utoaji wa huduma za afya na miradi mingine kudorora.

          Uwapo wa vita baridi miongoni mwa mataifa makubwa duniani pia kuliathiri sera za
          mambo ya nje za Tanzania. Hii ni kwa sababu nchi ilikuwa mwanachama wa Harakati
          za Kutofungamana na Upande Wowote (Non-Alignment Movement, NAM). Hali hii
          ilileta migogoro na mataifa makubwa yaliyokuwa yakihasimiana. Vilevile, utegemezi
          wa misaada kutoka nje ulipunguza uhuru wa taifa wa kupanga na kuamua mambo
          yake. Kwa mfano, mwaka 1965, Tanzania ilikumbwa na mgogoro wa kidiplomasia na
          Uingereza, hali iliyosababisha Uingereza kusitisha misaada. Hii iliathiri utekelezaji
          wa miradi mingi ya kimkakati nchini. Pamoja na changamoto hizi, mikakati ya awali
          ya ujenzi wa taifa iliweka msingi muhimu kwa juhudi za baadaye za maendeleo.




           Kazi ya kufanya 5.6


            Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mtandao na bainisha
            changamoto nyingine za ujenzi wa taifa na jinsi zilivyotatuliwa.










                                                  87




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   87
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   87                                         03/10/2024   18:15:19
   90   91   92   93   94   95   96   97   98   99   100