Page 93 - Historia_Maadili
P. 93

za kupata huduma bora, hasa katika utoaji wa mikopo. Aidha, baadhi ya watu ndani
          ya chama walionesha nia ya kupata uongozi ili kujinufaisha binafsi na kujilimbikizia
          mali. Baadhi ya mambo yaliyojitokeza baada ya uhuru ni kama yafuatayo:

           (a)  Kujengeka  kwa matabaka  ya kiuchumi,  kisiasa  na kijamii,  kinyume  na
                mfumo  wa kijamii  uliokuwepo  kabla  ya  uhuru ambapo  jamii  iliishi  kwa
        FOR ONLINE READING ONLY
                umoja, udugu, upendo na kushirikiana; na

           (b)  Baadhi ya viongozi na watumishi wa umma walianza kukiuka maadili ya

                utumishi wa umma na kutumia nafasi walizopewa kama vitega uchumi ili
                kujinufaisha wenyewe.
          Kutokana na kuongezeka kwa matabaka, ubadhirifu wa mali na baadhi ya viongozi
          wa umma kuanza kujilimbikizia mali, Serikali ya Awamu ya Kwanza ilichukua hatua

          ya kuunda tume. Mwaka 1966, Mwalimu Julius K. Nyerere aliunda Tume ya Rais
          ya Kudumu ya Uchunguzi (The Presidential Permanent Commission of Enquiry) ili
          kuchunguza mwenendo wa viongozi na watumishi wa umma waliokuwa wakikiuka
          maadili, kujilimbikizia mali na kutumia madaraka vibaya kinyume na miiko ya chama
          cha TANU, ambacho mara kwa mara kilikemea vitendo vya rushwa. Tume ya Rais ya
          Kudumu ya Uchunguzi ya mwaka 1966 ilichangia Kamati Kuu ya TANU kutangaza
          Azimio la Arusha mwaka 1967, lililoweka miiko mbalimbali yenye misingi ya utu na

          usawa katika jamii, mambo ambayo yalisaidia katika mapambano dhidi ya rushwa.

          Kwa upande wa Zanzibar, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iliweka sera ya umiliki
          wa ardhi chini ya tangazo la tarehe 8 Machi 1964. Kupitia tangazo hilo, Serikali ya
          Sheikh Abeid Amani Karume ilitaifisha mali zisizohamishika kama ardhi, mashamba
          na majengo na kuweka mpango wa ugawaji ardhi kwa utaratibu wa hekari tatu kwa
          kila familia. Sheria hiyo ilitoa fursa kwa ardhi iliyotaifishwa kugawanywa kwa
          familia na watu masikini wasio na ardhi. Kabla ya mapinduzi, asilimia kubwa ya

          ardhi, yakiwemo mashamba ya mikarafuu na minazi, ilikuwa ikimilikiwa na watu
          wachache hasa Waarabu.

          Ugawaji wa ardhi ulifanyika kupitia amri ya utaifishaji wa mali zisizohamishika, “The
          Confiscation of Immovable Property Decree 1964,” na amri ya ugawaji wa ardhi, “The
          Land Distribution Decree 1966.” Ugawaji huo ulianza huko Dole tarehe 11 Novemba
          1965, ambapo wananchi waligawiwa hekari tatu kila familia. Hadi kufikia mwaka
          1973, zaidi ya hekari 24,000 zilikuwa zimetolewa kwa Wazanzibari.







                                                  85




                                                                                        03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   85
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   85                                         03/10/2024   18:15:18
   88   89   90   91   92   93   94   95   96   97   98