Page 88 - Historia_Maadili
P. 88

mfumo mpya wa uchumi. Mifumo ya uchumi iliyobuniwa katika kipindi hiki ililenga
          kujenga jamii ya watu wanaojitegemea. Kwa mfano, Tanganyika ilianzisha Mpango
          wa Maendeleo wa Miaka Mitatu uliotekelezwa kuanzia mwaka 1961 hadi 1964.
          Baada ya mpango huo, ulianzishwa Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka
          Mitano (1964–1969), ambao ulitakiwa kufuatiwa na Mpango wa Pili wa Miaka
          Mitano. Mipango hii ililenga, miongoni mwa mambo mengine, kuleta maendeleo
        FOR ONLINE READING ONLY
          ya kiuchumi ya taifa huru.

          Kuanzia mwaka 1963 hadi 1965, sera ya maendeleo vijijini ilianzishwa. Hii ilikuwa
          ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitatu. Sera hii
          ililenga kuwaweka wananchi katika vijiji ili kuimarisha kilimo kwa kutumia teknolojia
          ya kisasa. Serikali iliamini kuwa kuwakusanya wananchi vijijini kungewezesha
          kurahisisha utoaji  wa huduma za ugani, elimu na miundombinu muhimu. Hii ilisaidia
          pia kuhamasisha maendeleo ya kilimo na kuwapa wananchi fursa ya kushiriki
          kikamilifu katika ujenzi wa taifa. Kilimo kilipewa kipaumbele na kuhimizwa kuwa
          uti wa mgongo wa taifa, huku wakulima wakihamasishwa kulima mazao ya biashara
          na chakula. Kupitia uhamasishaji huu, walipatiwa pembejeo na kupewa uhakika wa
          masoko ya mazao yao kupitia vyama vya ushirika.

          Vilevile, viwanda mbalimbali vilijengwa Tanganyika. Kwa mfano, Kiwanda cha
          Nguo cha Urafiki kilijengwa mwaka 1966 chini ya makubaliano ya urafiki kati ya
          Tanzania na China. Hiki kilikuwa kiwanda kamilifu chenye mitambo ya kisasa ya
          utengenezaji wa nguo. Viwanda vingine vingi katika kipindi hiki vilimilikiwa na
          wageni na vilijikita katika uzalishaji wa bidhaa kama vile vinywaji, uchakataji wa
          malighafi za kilimo na bidhaa za matumizi kama Coca-Cola, East African Breweries,
          Tanganyika Packers, British American Tobacco, Metal Box na Bata Shoes, Ubungo
          Fram Impelements na National Printing  Company.

          Aidha, serikali  ilijikita katika kuhakikisha taasisi za fedha zinaendelezwa ili kuwa
          mihimili muhimu katika ukuaji wa uchumi na maendeleo ya taifa. Serikali ilianzisha
          Benki Kuu ya Tanzania mwaka 1966 ili kusimamia masuala muhimu ya kifedha
          nchini. Pia sekta nyingine, kama vile uvuvi, nishati na madini, zilipewa kipaumbele.



           Kazi ya kufanya 5.3

            Tembelea wazee na watu wengine wenye ufahamu kuhusu mifumo ya uchumi
            iliyojengwa mara baada ya uhuru, kisha fanya mahojiano nao kuhusu mifumo
            hiyo kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
             (a)  Maisha ya jamii kiuchumi mara baada ya   uhuru;

             (b)  Mifumo ya kiuchumi iliyojengwa na jinsi ilivyoinufaisha jamii; na

             (c)  Andika ripoti ya uchunguzi wako.


                                                  80




                                                                                        03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   80                                         03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   80
   83   84   85   86   87   88   89   90   91   92   93