Page 84 - Historia_Maadili
P. 84

kisiasa, kijamii, kiutamaduni na kiuchumi kwa Taifa huru la Tanzania. Mifumo hiyo
          ilijengwa chini ya uongozi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa upande wa
          Tanganyika na Sheikh Abeid Amani Karume kwa upande wa Zanzibar. Katika kipindi
          hiki, vyama vya TANU na ASP vililenga kujenga taifa lenye kuzingatia maadili ya
          usawa, utu, heshima kwa kila mtu, haki na wajibu. Aidha, umoja, uzalendo, kujitolea
          na kupenda kazi vilikuwa miongoni mwa maadili yaliyojengwa, yakiongozwa na kauli
        FOR ONLINE READING ONLY
          mbiu iliyotangaza vita dhidi ya maadui watatu: umaskini, ujinga na maradhi. Kila
          mwananchi alisisitizwa kuzingatia maadili ya Kitanzania na kujiepusha na unyonyaji,
          rushwa, ukabila na uzembe. Mifumo ya kisiasa, kiuchumi na kijamii iliyojengwa
          katika kipindi hiki imefafanuliwa vema katika sehemu zinazofuata.



           Kazi ya kufanya 5.1


            Pitia mtandao au vifaa vingine vya TEHAMA, sikiliza hotuba za waasisi wa taifa
            ambao ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume
            kuhusu umuhimu wa maadili katika ujenzi wa taifa huru. Baada ya kusikiliza
            hotuba fanya yafuatayo:

             (a)  Bainisha mambo yaliyokugusa katika hotuba hizo.
             (b)  Kama ungekuwepo kipindi hicho ungependa  kuwauliza  mambo  gani
                  waasisi wa taifa letu?

             (c)  Eleza  namna maadili  yaliyozungumzwa  katika  hotuba hizo bado ni
                  muhimu katika Tanzania ya sasa.




          Kisiasa

          Tanganyika kuwa Jamhuri: Tanganyika ilikuwa Jamhuri mwaka 1962. Jamhuri
          ni serikali ya watu yenye mamlaka kamili, inayoongozwa na Rais. Msukumo wa
          Tanganyika kuwa Jamhuri ulitokana na sababu mbalimbali. Kwanza, ilihitajika kuwa
          na uhuru kamili wa serikali, badala ya kuwa na uhuru wa bendera chini ya uongozi
          wa Malkia wa Uingereza. Kabla ya Tanganyika kuwa Jamhuri, serikali ilikuwa
          inaongozwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kama Waziri Mkuu, aliyekuwa
          chini ya mamlaka ya Malkia wa Uingereza, huku Gavana wa kikoloni akiendelea kuwa
          kiongozi mkuu wa nchi, akimwakilisha Malkia Elizabeth II wa Uingereza. Gavana
          huyo aliendelea kutekeleza baadhi ya majukumu ya kiserikali, hivyo kumfanya Waziri
          Mkuu kukosa mamlaka kamili.
          Pia, Tanganyika ilitaka kutambulika katika jumuiya za kimataifa kama nchi yenye
          uhuru kamili na kuwa Jamhuri ilikuwa njia ya kufanikisha hilo, kwani iliwapa fursa ya
          kushiriki katika mikutano na jumuiya hizo za kimataifa. Vilevile, wananchi walitaka


                                                  76




                                                                                        03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   76
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   76                                         03/10/2024   18:15:17
   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88   89