Page 80 - Historia_Maadili
P. 80

wa Kijerumani na baadaye wa Kiingereza. Baadhi ya Watanzania waliochangia katika
          ujenzi wa uzalendo kwa jamii zao ni pamoja na Abushiri bin Salim al-Harthi wa
          Pangani, Mangi Meli wa Old Moshi, Mtemi Isike wa Unyanyembe, Mtwa Mkwawa
          wa Iringa, Mwene Machemba wa Wayao, Nkosi Songea, Mbano wa Wangoni na Liti
          Kidanka wa Singida.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Hivyo, harakati za wazalendo hawa kupinga uvamizi wa kikoloni, ulichangia katika

          ujenzi wa maadili ya uzalendo kwani wananchi walijitoa kushiriki katika vita na
          ulinzi wa jamii zao. Wanajamii walichangia ujenzi wa uzalendo pale walipopinga
          waziwazi sera za wakoloni na walipojitoa kushiriki katika vita dhidi ya wavamizi.
          Harakati za kupinga utawala na mifumo ya kikoloni zilipanda mbegu ya uzalendo
          kwa jamii za Kitanzania, kupenda jamii zao na hata kujitoa maisha yao kupambana
          dhidi ya uvamizi wa kikoloni. Hali hii ilichangia katika ujenzi wa kizalendo ndani
          ya jamii zao na baadaye kwa nchi nzima ya Tanzania.

          Vilevile, harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar nazo zilichangia katika

          ujenzi wa uzalendo miongoni mwa Watanzania. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
          na Sheikh Abeid Amani Karume pia walitoa mchango mkubwa nyakati zote za harakati
          za kudai uhuru. Walijitolea sehemu kubwa ya maisha yao kupigania uhuru wa
          Tanganyika na Zanzibar. Mwalimu Nyerere kwa upande wa Tanganyika alitoa
          mchango mkubwa katika kubadili TAA na kuanzishwa kwa TANU tarehe 7 Julai
          1954, kwani chama cha TAA kilikuwa na mwelekeo wa kijamii zaidi kuliko siasa.
          Pia, Mwalimu Nyerere  akiwa

          mwenyekiti wa  TANU na  Sheikh
          Karume akiwa mwenyekiti wa ASP
          walifanikiwa       kuwaunganisha
          viongozi na wananchi hadi kupatikana
          kwa uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
          mtawalia. Kielelezo 4.8 kinaonesha
          picha ya viongozi wakuu wa TANU
          na ASP, Mwalimu Julius Kambarage

          Nyerere na  Sheikh Abeid Amani  Kielelezo 4.8: Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
          Karume.                                     na Sheikh Abeid Amani Karume

          Aidha, viongozi wa vyama vya TANU na ASP pamoja na viongozi wengine katika
          ngazi mbalimbali walikuwa wazalendo, kwani walitoa mchango muhimu katika
          kuanzisha na kuendeleza harakati za kudai uhuru. Uzalendo wao ulidhihirika kupitia




                                                  72




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   72                                         03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   72
   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84   85