Page 76 - Historia_Maadili
P. 76
Chama cha ASP kilikuwa na malengo mengi, yakiwemo kupigania uhuru wa Zanzibar,
kuunda serikali ya kidemokrasia katika visiwa vya Unguja na Pemba, kuondoa ubaguzi
wa aina yoyote katika visiwa hivyo, kudumisha uhuru wa Zanzibar na watu wake,
pamoja na kuwaandaa wananchi wawe tayari kupigania uhuru wao.
Vyama vya siasa, hasa TANU kwa Tanganyika na ASP kwa Zanzibar, vilikuwa na
FOR ONLINE READING ONLY
mchango muhimu katika kukuza harakati za kupigania uhuru wa nchi hizo. Kwa
namna moja ama nyingine, vyama hivi viliunganisha wananchi na kuwaongoza
katika mapambano ya kuudai uhuru. Vilihamasisha wananchi kujiunga navyo na
kushiriki katika harakati za kuudai uhuru wa nchi zao. Viongozi wa TANU na ASP
walitangaza falsafa na sera za vyama hivyo kwa wanachama na wananchi wote kwa
ujumla. Pia, vyama hivi viliandaa mikutano ya kisiasa na kuhamasisha wanachama
pamoja na wananchi kuhudhuria mikutano hiyo.
Aidha, vyama vya siasa vilianzisha matawi katika maeneo mbalimbali ya nchi ili
kuvutia wanachama wengi zaidi. Vyama hivi vilitoa elimu na mafunzo ya kiuongozi
na kisiasa kwa viongozi wa matawi na ngazi ya kitaifa. Katika chaguzi mbalimbali
zilizofanyika kabla ya uhuru, vyama vya siasa vilishiriki na baadhi ya vyama
vilifanikiwa kupata wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria. Ni muhimu pia
kufahamu kuwa, vyama kadhaa, hasa TANU na ASP, vilianzisha vyombo vya habari
ili kuendeleza harakati za kudai uhuru. Kwa mfano, TANU kilianzisha gazeti lililoitwa
‘Sauti ya TANU’ na ASP kilianzisha
‘Sauti ya ASP.’ Hivyo basi, ni
dhahiri kuwa vyama vya siasa
vilichochea kukua kwa harakati za
kudai uhuru wa Tanganyika na
Zanzibar. Hata hivyo, vyama hivyo
vilikabiliana na changamoto nyingi,
ikiwemo upinzani mkali kutoka kwa
serikali ya kikoloni. Kielelezo 4.7
kinaonyesha picha ya Mwalimu
Nyerere akiwa na mawakili wake
wakielekea mahakamani kujibu kesi Kielelezo 4.7: Mwalimu Nyerere akiwa na
ya uchochezi. mawakili wakielekea mahakamani
Kazi ya kufanya 4.4
Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mtandao na bainisha mbinu
nyingine zilizotumika katika harakati za kuudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
68
03/10/2024 18:15:16
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 68 03/10/2024 18:15:16
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 68

