Page 72 - Historia_Maadili
P. 72
Kwa upande wa Tanganyika, mnamo mwaka 1935 ilianzishwa Klabu ya Waafrika
yenye jina la Young African Sports Club ambayo pamoja na kushiriki mashindano ya
mpira wa miguu ilikuwa na lengo la kuwaunganisha Waafrika kujadili masilahi yao,
matatizo yao na kuimarisha ushirikiano katika utatuzi wa changamoto mbalimbali.
Aidha, vilabu hivi vilichangia kwa kiasi kikubwa kuhamasisha wananchi kujiunga
FOR ONLINE READING ONLY
na Jumuiya za Waafrika kama vile; African Association, Shirazi Association na
TAA na baada ya jumuiya hizo kuwa vyama vya kupigania uhuru. Pia, vilabu hivi
vilitoa mchango mkubwa wa kuchangisha fedha kwa wanachama wao pamoja na
kuwahamasisha kujiunga na vyama vya TANU na ASP.
Kazi ya kufanya 4.3
Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mitandao, kisha fafanua jinsi
vikundi na vyama vya kidini vilivyochangia katika harakati za kudai uhuru wa
Tanganyika na Zanzibar.
Vyombo vya habari
Kuanzishwa kwa vyombo vya habari katika Tanganyika na Zanzibar kuliongeza na
kuimarisha harakati za Waafrika katika kupigania uhuru wao. Kabla ya kuanzishwa
kwa vyombo hivi vya Waafrika, kulikuwepo vyombo vya habari vilivyokuwa
vimeanzishwa na serikali ya kikoloni. Hata hivyo, vyombo hivyo vya kikoloni
havikutoa habari kuhusu harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, bali
vilijikita zaidi katika kuwasifia wakoloni na kuelezea matukio ya huko Ulaya.
Kutokana na changamoto hii, Waafrika wakaona kuwa kuna umuhimu wa kuunda
na kuanzisha vyombo vya habari vyao wenyewe. Mfano wa vyombo hivyo ni gazeti
la Kwetu, lililoanzishwa na jumuiya ya African Association (AA) mwaka 1937 na
Sauti ya TANU, ambalo lilihaririwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka
1957. Kazi hii ya uhariri ilimletea matatizo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
baada ya kuchapisha taarifa ambayo haikuupendeza utawala wa Waingereza. Hivyo,
mnamo tarehe 9 Julai 1958, Julius Kambarage Nyerere alishtakiwa katika Mahakama
ya Dar es Salaam kwa makosa ya uchochezi dhidi ya serikali ya kikoloni. Tarehe 12
Agosti 1958, Mwalimu Nyerere alihukumiwa kulipa faini ya shilingi elfu tatu, sawa
na paundi 150 za Uingereza, au kwenda jela miezi sita kama angeshindwa kulipa.
Wanachama na wapenzi wa TANU walichanga fedha na kumsaidia kulipa faini hiyo
ili kumnusuru Mwalimu Nyerere asitumikie kifungo cha jela.
64
03/10/2024 18:15:15
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 64
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 64 03/10/2024 18:15:15

