Page 77 - Historia_Maadili
P. 77

Zoezi la         4.3


            1.  Unafikiri  ni  kwa  nini  serikali  za  kikoloni  ziliwazuia Waafrika  kuanzisha
               vyama vya kisiasa?

            2.  Je,  unafikiri  ni  kwa  nini  vyama  vya  kiraia  vilivyoanzishwa  wakati  wa
        FOR ONLINE READING ONLY
               harakati za kudai uhuru vilibadilika na kuanza kujihusisha na siasa?

            3.  Eleza  mchango  wa vyama  vya  siasa  katika  harakati  za  kudai  uhuru wa
               Tanganyika na Zanzibar.
            4.  Fafanua mafanikio na changamoto zinazokabili vyama vya siasa kwa  sasa.

            5.  Eleza wajibu wa vyama vya siasa katika kuikuza demokrasia nchini.



          Mchango wa harakati za kupinga uvamizi na ukoloni
          Mchango wa harakati za kupinga uvamizi na ukoloni ulikuwa ni pamoja na kutunza
          maadili na kujenga uzalendo.

          Kutunza maadili
          Ujenzi wa maadili ni mchakato wa kihistoria kwa kuwa unatokana na hisia ambazo
          watu au jamii wamezikuza kwa miaka mingi kama sehemu ya harakati zao za kuleta
          maendeleo na uhuru katika jamii au nchi yao. Maadili ni muhimu kutunzwa kwa
          kuwa yanaleta fahari, umoja, ujasiri na mienendo inayokubalika katika jamii. Hivyo,
          harakati za kupinga ukoloni nazo zilichangia katika utunzaji wa utambulisho wa
          Mtanzania, ambao ni pamoja na umoja, utu, mshikamano na lugha ya Kiswahili.


          Umoja
          Harakati za kupinga uvamizi na mifumo ya kikoloni zilichangia pia katika kudumisha
          maadili ya umoja miongoni mwa jamii za Kitanzania. Kabla ya ukoloni, jamii za
          Kitanzania zilikuwa zimegawanyika katika makabila mbalimbali. Kila kabila lilikuwa
          na utaratibu wake wa maisha, ikiwa ni pamoja na mila na desturi zake. Pia, inapaswa
          kukumbukwa kuwa wakoloni walikuwa na nguvu kubwa za kijeshi na walimiliki
          silaha bora zaidi ikilinganishwa na silaha za jadi zilizotumiwa na jamii za Kitanzania
          wakati huo. Hivyo, viongozi wa jamii mbalimbali za Kitanzania walihimiza umoja
          miongoni mwa wanajamii ili kuwa na nguvu ya kukabiliana na uvamizi na utawala
          wa kikoloni. Waliamini kuwa “umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu.”

          Aidha, kuelekea kipindi cha kupata uhuru, kwa mfano, viongozi kama Mwalimu Julius
          Kambarage Nyerere, Sheikh Abeid Karume na wengineo waliunganisha makabila
          na jamii mbalimbali. Hali hii, ilisaidia kuendeleza mapambano ya ukombozi kwa
          pamoja kama jamii moja ya Watanganyika na jamii ya Wazanzibari  katika kudumisha



                                                  69




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   69
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   69                                         03/10/2024   18:15:16
   72   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82