Page 82 - Historia_Maadili
P. 82

Kazi ya kufanya 4.5


            Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mitandao, kisha bainisha jinsi
            maadili mengine ya Kitanzania yaliyotunzwa wakati wa harakati za kudai uhuru
            wa Tanganyika na Zanzibar.
        FOR ONLINE READING ONLY

                              Zoezi la         4.4



            1.  Eleza jinsi maadili ya kikoloni yalivyoathiri maadili ya jamii za Kitanzania
               wakati wa ukoloni.
            2.  Kwa kurejea muktadha wa kipindi cha kupigania uhuru wa Tanganyika na
               Zanzibar. Fafanua misingi ya usemi kuwa, “umoja ni nguvu, utengano ni
               udhaifu”.

            3.  Pendekeza mikakati ya kudumisha maadili yaliyotunzwa wakati wa harakati
               za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.
            4.  Eleza mikakati ya kujenga uzalendo kwa vijana katika mazingira ya sasa.



                                    Zoezi la  marudio



            1.  Je, unafikiri ni kwa nini harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
                zilifanikiwa kuwaunganisha wananchi?

            2.  Kwa nini  vyama  vya TANU na ASP vilipata  uungwaji  mkono  mkubwa
                ukivilinganisha na vyama vingine vya siasa wakati wa kupigania uhuru?


            3.  Eleza mchango wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid
                Amani Karume katika kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.

            4.  Eleza kwa nini uhuru wa Tanganyika na Zanzibar unapaswa kulindwa.

            5.  Fafanua maadili yaliyodumishwa wakati wa harakati za kudai uhuru wa
                Tanganyika na Zanzibar.


            6.  Kwa kutumia mifano, eleza maana ya uzalendo.

            7.  Jadili mchango wa viongozi wa kisiasa wa sasa katika kutunza maadili na
                kujenga uzalendo.



                                                  74




                                                                                        03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   74
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   74                                         03/10/2024   18:15:17
   77   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87