Page 87 - Historia_Maadili
P. 87

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Tarehe 26 Aprili, 1964, ni tukio muhimu
          la kihistoria na kisiasa katika kipindi hicho. Muungano huu ulitokana na uhusiano
          wa kihistoria uliokuwepo kati ya jamii za Tanganyika na Zanzibar, uhusiano ambao
          ulitokana kwa kiasi kikubwa na udugu, historia na biashara uliojengwa karne nyingi
          kabla ya ukoloni. Aidha, Muungano huu ulikuwa nguzo muhimu katika kulinda
          uhuru na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Muungano huu uliunda utaifa mpya wa
        FOR ONLINE READING ONLY
          Utanzania.

          Uanzishwaji wa mfumo wa chama kimoja cha kisiasa mwaka 1965: Tanzania iliamua
          kufuta  mfumo wa vyama vingi na kuanzisha mfumo wa chama kimoja. Vyama
          vilivyoruhusiwa kufanya siasa vilikuwa ni TANU kwa Tanganyika na ASP kwa
          upande wa Zanzibar. Sababu ya kuanzisha mfumo wa chama kimoja ilikuwa ni kuleta
          maendeleo na kuudumisha umoja na mshikamano. Uanzishwaji wa mfumo huu
          ulienda sambamba na uanzishwaji wa siasa ya ujamaa na kujitegemea mwaka 1967.



                              Zoezi la          5.1



            1.  Pendekeza mikakati ya kuboresha mfumo wa  ubalozi wa nyumba kumi
               katika kuimarisha ulinzi na usalama kwenye  mazingira unayoishi.
            2.  Kwa nini sera ya Afrikanaizesheni ilikuwa muhimu mara baada ya uhuru wa
               Tanganyika na Mapinduzi ya Zanzibar?

            3.  Eleza umuhimu wa kuwa na vijana wenye uzalendo katika taifa.

            4.  Eleza umuhimu wa Jeshi la Kujenga Taifa katika kujenga maadili ya vijana
               wa Kitanzania.



          Uchumi na huduma za jamii

          Mara baada ya uhuru, serikali iliweka mkazo katika kujenga mifumo imara ya uchumi
          na huduma za jamii. Harakati za kujenga mifumo hii ziliongozwa na nadharia ya
          kupambana na maadui watatu: ujinga, maradhi na umasikini. Kuwapo kwa ujinga,
          maradhi na umasikini kulisababishwa na mifumo ya kiuchumi na kijamii iliyojengwa
          wakati wa ukoloni. Hivyo, katika kipindi hiki, kulikuwa na umuhimu wa kujenga na
          kuimarisha uchumi na huduma za jamii.

          Uchumi
          Mara baada ya uhuru, Tanganyika na Zanzibar zilirithi mfumo wa uchumi wa kikoloni
          ambao ulinufaisha watu wachache, wengi wao wakiwa wageni. Uchumi huu haukuwa
          na uwiano wa maendeleo; kulikuwa na maendeleo hafifu katika sekta ya kibiashara,
          huku sekta ya viwanda ikiwa ndogo na kumilikiwa na wageni. Kulihitajika kujenga


                                                  79




                                                                                        03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   79
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   79                                         03/10/2024   18:15:17
   82   83   84   85   86   87   88   89   90   91   92