Page 89 - Historia_Maadili
P. 89

Huduma za jamii
          Mabadiliko katika utoaji huduma za jamii yalilenga kubadilisha mfumo wa kikoloni na
          kuunda mfumo unaokidhi mahitaji ya taifa huru. Mfumo mpya wa utoaji huduma za
          jamii ulilenga kujenga jamii yenye ujuzi, maarifa na afya katika ujenzi wa taifa huru.

          Mara baada ya uhuru vipaumbele vya elimu vilibadilika kuendana na matakwa ya
        FOR ONLINE READING ONLY
          nchi. Baada ya uhuru, wataalamu wengi Wazungu waliondoka, hivyo watumishi
          Waafrika walibaki wachache. Hii ilileta umuhimu wa kuwaandaa wataalamu wazawa.
          Kwa maana hiyo, serikali ilijikita kutoa elimu kwa wote iliyokuwa na lengo la kufanya
          kila raia anakuwa na ufanisi katika kazi zake za kila siku na inayoweza msaidia
          kujiendeleza zaidi kielimu. Hii ilitekelezwa zaidi upande wa elimu ya msingi ambapo
          shule mpya zilijengwa na kuongeza idadi ya wanafunzi. Pia, Mpango wa Kwanza wa
          Miaka Mitano ulijikita katika upanuzi wa elimu ya sekondari ili kuandaa wataalamu
          na viongozi wa baadaye, ingawa changamoto za rasilimali na walimu zilikuwepo.
          Pamoja na hayo, elimu hii ilitolewa kwa watu wote bila kujali jinsia, ukanda, hadhi
          au kabila tofauti na elimu ya kikoloni. Serikali ilianzisha na kujenga shule mpya na
          kuongeza idadi ya wanafunzi waliojiunga na elimu ya sekondari.

          Vilevile, serikali ilianzisha vyuo vya ufundi ili kutoa mafunzo ya ufundi na ufundi
          stadi kwa vijana, jambo ambalo lilikuwa muhimu kwa kuimarisha sekta ya viwanda
          na kilimo. Kwa mfano, Chuo cha Ufundi Dar es Salaam, ambacho kilipanuliwa mwaka
          1962 na kuanza kutoa elimu ya ufundi mwaka 1964. Aidha vyuo vya ualimu vilianzishwa
          na kupanuliwa. Baadhi ya vyuo hivyo ni Chuo cha Ualimu Morogoro (Kigurunyembe)
          ambacho hapo mwanzo kilimilikiwa na Wamisionari. Chuo hiki kilijikita katika kuandaa
          walimu wa kwenda kufundisha shule za msingi ili kuendana na upanuzi wa shule za msingi
          nchini walipoanzisha Daraja la IIIA mwaka 1961 na Diploma (stashahada) baadae mwaka
          1970 baada ya kupandishwa hadhi na kuanza kutoa mafunzo ya  Diploma (stashahada)
          mwaka 1966.

          Maendeleo katika sekta ya elimu hayakuishia katika kada za chini na kati tu, bali
          yalienda hadi katika elimu ya juu. Kwa mfano, mwaka 1961 serikali ilikianzisha
          Chuo Kikuu Kishiriki cha Dar es Salaam (University College of Dar es Salaam) chini
          ya Chuo Kikuu cha London. Hii ilikuwa hatua muhimu katika kuandaa wasomi na
          wataalamu mbalimbali wa ngazi ya juu.

          Upanuzi wa miundombinu ya afya, ikijumuisha ujenzi wa zahanati na hospitali za
          umma vijijini na mijini. Upanuzi mkubwa ulikuwa ni ule wa  Hospitali ya Muhimbili
          mnamo  mwaka 1961 mara baada ya uhuru. Upanuzi huu ulisababisha kubadili jina
          toka Hospitali ya Princess Margareth na kuwa Hospitali ya Muhimbili. Hii ilikuwa
          hatua kubwa sana katika sekta ya afya. Pia, serikali ilijenga na kupanua hospitali za
          kikanda na pia kujenga vituo vya afya na zahanati katika maeneo ya mijini na vijijini.
          Lengo lilikuwa kufikisha huduma kwa wananchi wengi, hususani wale wa maeneo ya
          vijijini ambao awali walikuwa hawapati huduma bora za afya. Juhudi hizi zilihusisha
          kuajiri na kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya.


                                                  81




                                                                                        03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   81                                         03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   81
   84   85   86   87   88   89   90   91   92   93   94