Page 90 - Historia_Maadili
P. 90

Aidha, uanzishwaji programu za mafunzo ya wahudumu wa afya na madaktari.
          Hii ilijumuisha ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wa tiba na wahudumu wa afya
          waliokuwa wakipelekwa nje ya nchi kwa mafunzo ya juu. Vilevile, serikali ilijitahidi
          kuleta vifaa tiba na dawa kutoka nje ya nchi ili kuongeza ubora wa huduma zilizokuwa
          zinatolewa. Juhudi zote hizi ziliwezesha kuboresha hali ya afya kwa ujumla, kuweka
          mfumo wa afya wakushughulikia changamoto mbalimbali za kiafya.
        FOR ONLINE READING ONLY

                              Zoezi la          5.2


            1.  Eleza umuhimu wa elimu katika kujenga taifa lenye umoja, amani na
               mshikamano mara baada ya uhuru.
            2.  Chambua mchango wa huduma za jamii  katika  kukuza uchumi wa nchi
               mara baada ya uhuru.

            3.  Linganisha mikakati ya utoaji huduma za jamii mara baada ya uhuru na sasa.



          Utamaduni na maadili

          Utamaduni ni mfumo wa maisha unaojengwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja
          hadi kingine kupitia malezi, elimu na mawasiliano ndani ya jamii. Unajumuisha
          imani, maadili, mila na desturi, lugha, sanaa, muziki, mavazi, chakula na tabia ambazo
          zinaainisha na kuunganisha kundi fulani la watu. Katika kipindi cha uhuru, utamaduni
          ulikuwa na jukumu muhimu katika kuunda na kujenga taifa. Moja ya hatua kubwa
          zilizochukuliwa na serikali katika kipindi hicho ilikuwa kuifanya lugha ya Kiswahili
          kuwa lugha rasmi ya taifa. Wakati huo, Kiswahili hakikutumika tu kama chombo
          cha mawasiliano, bali pia kama njia ya kuhifadhi na kueneza maarifa, maadili na
          historia ya jamii.

          Pia, serikali ilianzisha vyombo mbalimbali vya kusimamia sanaa na michezo ili
          kulinda na kukuza utamaduni wetu. Ilianzisha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA),
          Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Bodi
          ya Filamu Tanzania, Makumbusho ya Taifa na vyama mbalimbali vya kusimamia
          michezo kama mpira wa miguu, pete, kikapu, ndondi na riadha.

          Aidha, sanaa na muziki ni sehemu nyingine muhimu ya utamaduni iliyopewa uzito
          kipindi hiki. Sanaa kama vile uchoraji, uchongaji, ngoma na nyimbo hutumiwa
          kuelezea hisia, mawazo na historia ya jamii. Muziki ulitumika kuelezea maadili na
          mapambano yaliyofanywa kulikomboa taifa. Vilevile, sanaa na muziki vilitumika
          kuamsha hisia za umoja na fahari ya taifa. Wasanii na waandishi wa vitabu walihimizwa
          kutumia kazi zao kuelimisha umma kuhusu ujenzi wa taifa. Bendi mbalimbali za
          muziki zilianzishwa na nyingine kuimarishwa. Baadhi ya bendi hizo ni kama NUTA
          Jazz Band (1964), Dar es Salaam Jazz Band, Kilwa Jazz Band, Morogoro Jazz Band,

                                                  82




                                                                                        03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   82
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   82                                         03/10/2024   18:15:18
   85   86   87   88   89   90   91   92   93   94   95