Page 85 - Historia_Maadili
P. 85

Serikali ya Jamhuri ili kuwa na uwezo wa kuingia mikataba ya kimataifa kama nchi
          huru na yenye mamlaka yake kamili. Sababu nyingine ya kuunda Jamhuri ilikuwa
          ni kuwaondoa  Wazungu katika nafasi za juu za uongozi na kuruhusu Watanganyika
          kushika madaraka ya uongozi wa taifa lao. Baada ya Tanganyika kupata uhuru,
          Waingereza walikuwa bado wameshikilia baadhi ya nafasi za uongozi na waliendelea
          kutoa miongozo katika utawala wa nchi, hali iliyowafanya Watanganyika wajihisi
        FOR ONLINE READING ONLY
          kuwa bado wapo chini ya utawala wa kikoloni. Wananchi wa Tanganyika walitaka
          kufanya uamuzi bila kuingiliwa na wakoloni, kwani viongozi wa serikali hawakuwa
          na uhuru wa kufanya uamuzi wa kiutawala kabla ya kuwa Jamhuri.

          Aidha, nchi kuwa Jamhuri kulilenga kuwapa uhuru wananchi na viongozi kujitawala
          na kuharakisha maendeleo ya taifa. Jamhuri ilileta umoja na mshikamano, ikitokomeza
          misingi ya ukabila na udini ambayo ilitumiwa na wakoloni kuwatenganisha
          Watanganyika, hivyo kuwapa nafasi ya kujiletea maendeleo kwa kasi zaidi. Baada ya
          Tanganyika kuwa Jamhuri, Mwalimu Nyerere aliunda baraza la kwanza la mawaziri,
          kama baadhi yao wanavyoonekana katika Kielelezo 5.1.



           Kazi ya kufanya 5.2

              Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwamo mtandao ili kubainisha
              majina ya mawaziri wa Baraza la Mawaziri la kwanza la Tanganyika mwaka
              1961.































                    Kielelezo 5.1: Baraza la Kwanza la Mawaziri la Tanganyika mwaka 1961




                                                  77




                                                                                        03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   77
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   77                                         03/10/2024   18:15:17
   80   81   82   83   84   85   86   87   88   89   90