Page 83 - Historia_Maadili
P. 83

Sura ya Tano                        Ujenzi wa taifa baada

                                                          ya ukoloni


        FOR ONLINE READING ONLY

                   Utangulizi



            Mara tu baada ya kupata uhuru, kilianza kipindi cha mpito kutoka katika
            harakati za kudai uhuru hadi kuanzishwa kwa harakati mpya za ujenzi wa taifa
            huru. Katika sura hii, utajifunza dhana ya ujenzi wa taifa, mifumo ya kiuchumi,
            kisiasa, kijamii na kimaadili iliyojengwa kuanzia mwaka 1961 hadi 1966. Pia,
            utajifunza mikakati na changamoto zilizokuwapo katika harakati za ujenzi wa
            taifa. Umahiri utakaoujenga utakuwezesha kulinda na kuthamini juhudi za
            ujenzi wa taifa zilizoanzishwa na waasisi wa taifa letu.





                   Fikiri



             Hali ya taifa letu mara baada ya uhuru.



          Dhana ya ujenzi wa taifa

          Ujenzi wa taifa ni mchakato unaohusisha juhudi za pamoja za kuunda taifa jipya lenye
          utambulisho wake kupitia mifumo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni,
          unaozingatia haki, usawa na demokrasia. Katika taifa la Tanzania, mfumo huu
          ulijengwa juu ya misingi ya kiitikadi, fikra, falsafa na maadili ya jamii za Kitanzania.
          Harakati za ujenzi wa taifa zilikuwa muhimu kwa sababu ukoloni uliacha jamii
          iliyogawanyika, yenye ukosefu wa miundombinu muhimu, rasilimali watu na pia
          tofauti za kiuchumi na kijamii miongoni mwa wananchi. Harakati za ujenzi wa taifa
          baada ya ukoloni zililenga kujenga umoja wa kitaifa, uchumi imara, demokrasia,
          maadili na ustawi wa wananchi wote. Aidha, harakati hizi zililenga kuondoa mabaki
          na kasumba za mifumo ya utawala wa kikoloni iliyokuwa imeigawa jamii katika
          misingi ya rangi, kikabila, kidini na kikanda.

          Mifumo iliyojengwa kati ya  mwaka 1961 hadi 1966

          Uhuru wa Tanganyika wa Desemba 9, 1961, pamoja na Mapinduzi Matukufu ya
          Zanzibar ya Januari 12, 1964, yaliashiria mwanzo wa ujenzi wa mifumo mipya ya


                                                  75




                                                                                        03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   75                                         03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   75
   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88