Page 78 - Historia_Maadili
P. 78

maadili ya umoja yaliyodumu kwa muda mrefu. Maadili haya ya umoja yalikuwa
          muhimu katika kujenga mshikamano miongoni mwa jamii za Kitanzania.  Pia, ilisaidia
          kudumisha nguvu ya kitaifa, kupinga ukoloni na kudai uhuru wa Tanganyika na
          Zanzibar. Kwa hivyo, harakati za kupinga uvamizi na utawala wa kikoloni na juhudi
          za kudai uhuru, zilichangia katika kudumisha maadili ya umoja na nguvu ya kitaifa
          katika kudai uhuru wa nchi zao.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Utu
          Uvamizi na utawala wa kikoloni ulikuwa ni wa kimabavu na uliweka mifumo ya
          kuwanyanyasa, kuwanyonya na kuwakandamiza Watanzania. Hali hii ilitweza utu
          wao. Pia, Watanzania walidhalilishwa kwa adhabu kali za viboko hadharani pale
          waliposhindwa kulipa kodi au kufanya makosa mengine. Adhabu hizi zilitolewa kwa
          kuwavua nguo na kuwachapa mijeledi hadharani, kitendo kilichowachukiza sana
          wananchi kwa kuwa kilitweza na kudhalilisha utu wao.

          Kwa sababu hii, wananchi walipinga na kupambana ili kuonesha hisia zao za
          kuchoshwa na dhuluma na manyanyaso ya wakoloni. Harakati mbalimbali dhidi ya
          uvamizi na matendo maovu ya wakoloni zilitokea karibu kila sehemu ya Tanganyika.
          Ukoloni na mifumo yake iliathiri sana utu wa Waafrika na hivyo kuamsha ari ya
          kupata uhuru ili kutunza maadili ya utu yaliyokuwa yamejengwa na jamii za asili
          za Tanganyika na Zanzibar. Kwa hivyo, harakati za kupinga ukoloni pia zilichangia
          katika utunzaji na udumishaji wa maadili ya utu, kwani Watanzania hawakuwa tayari
          kuona utu wao au maadili yao yakipotea.

          Mshikamano
          Harakati za kupinga ukoloni na kupigania uhuru wa  Tanganyika na Zanzibar
          zilichangia pia katika kutunza maadili ya mshikamano miongoni mwa jamii za
          Kitanzania. Wakati wa kupinga uvamizi, viongozi waliwaunganisha watu katika
          jamii zao ili kuwa na nguvu za kupambana na uvamizi wa wakoloni. Viongozi wa
          jamii kama vile Mtwa Mkwawa wa kabila la Wahehe, Mangi Meli wa Old Moshi,
          Mtemi Isike wa Unyanyembe na viongozi wengine walihamasisha watu wao
          kushikamana ili kukabiliana na uvamizi wa wakoloni wa Kijerumani. Viongozi
          hawa walitambua kwamba adui yao alikuwa na nguvu za kijeshi. Hivyo, jamii zao
          zilihitaji mshikamano ili kuweza kupambana na wakoloni hao. Kuyatunza maadili ya
          mshikamano kuliwawezesha kutoa upinzani mkali kwa wavamizi, ingawa baadaye
          hawakufanikiwa  kutokana na sababu mbalimbali.

          Aidha, wakati wa harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, viongozi
          walihimiza mshikamano wa Watanzania wote ili kuwezesha Tanganyika na Zanzibar
          kupata uhuru. Katika kuimarisha mshikamano dhidi ya utawala wa Waingereza,
          wananchi walijiunga katika makundi mbalimbali ya kimasilahi, ambapo wakulima
          wa mazao makuu ya biashara waliunda vyama vya ushirika kupigania bei nzuri ya



                                                  70




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   70                                         03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   70
   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83