Page 75 - Historia_Maadili
P. 75

Vyama vya siasa
          Umoja wa Waafrika ulioitwa African Association (AA) uliundwa mwaka 1929 na
          mnamo mwaka 1948 ulipewa jina jipya la Tanganyika African Association (TAA).
          Mwaka 1954, chama hiki kilibadilishwa jina tena na kuwa chama rasmi cha siasa
          kwa jina la TANU.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Chama cha TANU kilikuwa na malengo mengi na baadhi ya malengo hayo yalikuwa
          ni pamoja na kuwaunganisha wananchi wa Tanganyika na kuwaongoza katika
          mapambano ya kupigania uhuru wa nchi yao, kutoa tafsiri mpya ya ukombozi, kuweka
          juhudi na fikra mpya za mapambano kwa misingi ya kifalsafa, pamoja na kudai haki
          ya kuwa na wawakilishi wa kidemokrasia katika vyombo vya kutunga sheria.

          Mbali na chama cha TANU, kulikuwa na vyama vingine vya kisiasa wakati wa
          harakati za kupigania uhuru. Mfano wa vyama hivyo ni United Tanganyika Party
          (UTP) kilichoanzishwa mwaka 1956, ambacho kiliungwa mkono na Wazungu, Waasia
          na baadhi ya Waafrika, hasa machifu. Vyama vingine ni African National Congress
          (ANC), kilichojitenga kutoka TANU mwaka 1958 na kuongozwa na Zuberi Mtemvu.
          ANC ilipingana na TANU katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika, hasa katika
          suala la kupiga kura tatu ambalo mwalimu Nyerere na wanachama wengine wenye
          msimamo wa kati walilikubali, huku Zuberi Mtemvu na wanachama wengine wenye
          msimamo mkali walilikataa na kuamua kujitenga. Pia, chama cha All Muslim National
          Union of Tanganyika (AMNUT) kilikuwa chama cha nne kuanzishwa Tanganyika.
          Kama ilivyokuwa TANU, AMNUT pia kilidai uhuru lakini walitaka mabadiliko ya
          katiba na uhuru viletwe polepole na si haraka kama TANU ilivyotaka. Mpaka wakati
          wa uhuru, Tanganyika ilikuwa na vyama hivi vinne.
          Kwa upande wa Zanzibar, vyama vilivyojitokeza kudai uhuru ni pamoja na Zanzibar
          Nationalist Party (ZNP) kilichoanzishwa mwaka 1955, Afro-Shirazi Party (ASP)
          kilichoanzishwa mwaka 1957 na  Zanzibar and Pemba People’s Party (ZPPP)
          lililoundwa mwaka 1959. Vyama vyote hivi vilikuwa na lengo kuu la kudai uhuru wa
          Wazanzibari, ingawa viliungwa mkono
          na wanachama wa rangi tofauti.

          Chama cha  ASP kiliundwa baada
          ya kuunganishwa kwa vyama viwili
          vilivyokuwepo hapo awali, yaani African
          Association na Shirazi Association. Baada
          ya kuundwa kwa chama cha ASP, Sheikh
          Abeid  Amani Karume alichaguliwa
          kuwa Rais wa ASP, Mtoro Rehani Kingo
          alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais na
          Thabiti Kombo Jecha alichaguliwa kuwa
          Katibu Mkuu. Kielelezo 4.6 kinaonesha
          picha ya Thabit Kombo Jecha.                  Kielelezo 4.6: Thabit Kombo Jecha


                                                  67




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   67                                         03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   67
   70   71   72   73   74   75   76   77   78   79   80