Page 73 - Historia_Maadili
P. 73

Kwa upande wa Zanzibar, kulikuwepo na vyombo vya habari kama magazeti na
          majarida mbalimbali, kwa mfano, gazeti la Sauti ya Zanzibar (1949), gazeti la
          Samachar lililoandikwa na Bwana Mtoro bin Abu Rehan, jarida la African Events na

          Alfalaq (1929) lililoandikwa na Ahmed Yahya Aldarda. Magazeti mengine ni Afrika
          Kwetu, Muongozo, Jasho Letu, Mkombozi, Mwiba, Sauti ya Afro-Shirazi, Sauti ya
        FOR ONLINE READING ONLY
          Jogoo na Umma.

          Vyombo vya habari vya Waafrika vililenga kuamsha ari ya uzalendo kwa Watanganyika

          na  Wazanzibari ili kuwaunganisha
          katika kudai uhuru wao. Vilikuwa na
          jukumu la kutoa elimu ya uzalendo na
          kuwaelimisha wananchi kuhusu sera

          na itikadi za vyama kama  TANU na
          ASP. Aidha, vilitumika kuhamasisha na
          kupaza sauti dhidi ya maovu yaliyokuwa
          yakifanywa na serikali za kikoloni.

          Kielelezo 4.4 kinaonesha mojawapo ya
          ukurasa wa mbele wa gazeti la Sauti ya
          TANU.                                       Kielelezo 4.4: Gazeti la Sauti ya TANU


          Vikundi na vyama vya sanaa


          Wakati wa utawala wa kikoloni, hakukuwa na nafasi ya kutosha kwa Watanganyika
          na Wazanzibari kusimama na kujieleza kwa uhuru kuhusu haki zao na harakati za
          ukombozi. Badala yake, mambo mengi
          ya harakati za  Watanganyika na
          Wazanzibari kudai uhuru yalifanyika kwa

          siri kuhofia adhabu kutoka kwa wakoloni.
          Viongozi na wanachama wa TANU na
          ASP waliamua kutumia sanaa na michezo

          kama mbinu mbadala.

          Sanaa  ilitumika  katika  kukuza  na
          kuendeleza harakati za kudai uhuru wa
          Tanganyika na Zanzibar. Watanganyika       Kielelezo 4.5: Bibi Titi Mohamed akiwa

          walianzisha vikundi na vyama vya sanaa                  jukwaani


                                                  65




                                                                                        03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   65                                         03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   65
   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77   78