Page 71 - Historia_Maadili
P. 71

ukombozi cha Afro-Shirazi Party (ASP) ambacho
          pia ndicho kilichoungana na TANU kuunda Chama
          Cha Mapinduzi mwaka 1977.

          Pamoja na kutetea haki na masilahi ya

          wafanyabiashara, vyama hivi vilikuja kushiriki katika
        FOR ONLINE READING ONLY
          harakati za kudai uhuru, ikiwa ni pamoja na baadhi
          yao kubadilika na kuwa vyama vya kisiasa. Kielelezo
          4.3 kinaonesha picha ya Abdulwahid Kleist Sykes.
                                                               Kielelezo 4.3: Abdulwahid Kleist
                                                                          Sykes
          Vikundi na vyama vya kidini
          Dini za Kikristo na Kiislamu zilitumika kama vyombo vya kuwaunganisha watu na
          kuendeleza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibari. Vyama na vikundi

          vya kidini vya Waafrika vilianzishwa kwa lengo la kupigania haki, usawa na uhuru
          wa kuabudu, pamoja na kudumisha utamaduni wa Watanganyika na Wazanzibari.
          Miongoni mwa vikundi na vyama vya kidini vilivyoanzishwa nchini Tanganyika ni
          Al-Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (1933), The Watch Tower Church, The African
          National Church na The Church of God.

          Al-Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilitoa viongozi shupavu kama Ally Sykes, Bibi
          Titi Mohamed, Tewa Said Tewa na wazalendo wengine ambao baadaye walishirikiana

          na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.
          Kwa upande wa Zanzibar, kulikuwa na Jumuiya iliyoitwa Jamiyatu Shubbaniul
          Muslimin, iliyoanzishwa tarehe 25 Novemba 1935 huko Gulioni, Unguja na Sheikh
          Salim Bin Abdullah Al Wadan (1901 - 1941), kwa lengo la kupinga mila na desturi
          za Kizungu.


          Vilabu vya mpira wa miguu
          Vilabu vya mpira wa miguu vya Waafrika vilianzishwa na kusaidia kuimarisha umoja
          na mshikamano miongoni mwa Waafrika sambamba na kueneza fikra za ukombozi
          dhidi ya madhila ya ukoloni. Vilabu hivyo viliweza kuonesha ushindani mkubwa

          dhidi ya vilabu vilivyosimamiwa na wakoloni na hivyo kuamsha ari kwa Waafrika ya
          kupambania haki zao za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Mwaka 1931 ilianzishwa klabu
          ya mpira wa miguu Zanzibar kwa jina la The African Sports Club ambayo kiongozi
          wake alikuwa Sheikh Abeid Amani Karume. Aidha, Klabu hii ilikuwa msingi wa
          kuanzishwa kwa Jumuiya ya Waafrika (African Association) mwaka 1933 ambayo
          iliwaunganisha Waafrika wa Unguja na Pemba kudai haki zao mbalimbali.


                                                  63




                                                                                        03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   63                                         03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   63
   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75   76