Page 69 - Historia_Maadili
P. 69

Vyama vya wafanyakazi

          Waafrika waliokuwa wameajiriwa katika viwanda, mashamba, bandari na sehemu
          nyingine walianzisha vyama vyao vya wafanyakazi kwa lengo la kulinda na kutetea
          masilahi yao ya kikazi. Malengo hayo yalijumuisha kudai kulipwa mishahara kwa
          wakati, ujira unaostahili na mazingira bora ya kazi. Madai mengine yalikuwa ni
        FOR ONLINE READING ONLY
          kupinga ubaguzi na unyanyasaji kazini, kupunguza masaa au muda wa kazi na kupinga
          kodi za kinyonyaji.

          Mfano wa vyama hivyo ni Tanganyika Territory Civil Servants’ Association (TTCSA),
          kilichoanzishwa na Martin Kayamba mwaka 1922 huko Tanga, ambacho mwaka
          1924 kilifungua tawi lake mjini Dar es
          Salaam. Pia, ndani ya kipindi hicho cha
          mwaka 1922 wafanyakazi wa serikali wa
          Dar es Salaam walianzisha  Tanganyika
          African Government Servants Association
          (TAGSA). Vyama vingine vilivyoundwa
          ni pamoja na  Association of Cooks  and
          Washmen (1939),  Dock Workers’ Union
          (1937), Railway African Civil Service Union
          (1920) na Tanganyika Federation of Labour
          (1955) chini ya uongozi wa Rashid Mfaume
          Kawawa. Kielelezo 4.2 kinaonesha picha ya         Kielelezo 4.2: Rashid Mfaume
          Rashid Mfaume Kawawa.                                      Kawawa

          Kwa upande wa Zanzibar, mnamo mwaka 1939, Sheikh Abeid Amani Karume aliunda
          Jumuiya ya Mabaharia kwa ajili ya kupigania haki za wafanyakazi katika vyombo
          vya baharini. Ambapo mwaka 1941, Jumuiya ya Mabaharia, Jumuiya ya Wachukuzi
          na Umoja wa Watumishi wa Nyumba za Wazungu walikutana kujadili mikakati ya
          ukombozi dhidi ya unyonyaji kazini. Baadaye, mwaka 1948, Chama cha Masonara,
          Chama cha Wafanyakazi wa Hospitali na Chama cha Mafundi wa Majahazi pia
          vilikutana kwa lengo la kujadili namna ya kutetea masilahi yao katika sehemu za kazi.

          Aidha, Baraza la Umoja wa Vijana wa Kiafrika (Youth African Council Union)
          liliundwa mwaka 1949. Baraza hili lilianzishwa kwa madhumuni ya kupigania haki
          ya kupata kazi na mishahara inayolingana na elimu na ujuzi wa mtu. Hata hivyo,
          mnamo mwaka 1956, Muungano wa Vyama vya Wafanyakazi wa Zanzibar na Pemba
          (Federation of Zanzibar and Pemba Trade Unions - ZPFL) ulianzishwa.

          Pamoja na juhudi zao za kutetea masilahi ya wafanyakazi, waliendelea kujadili
          masuala ya kisiasa na hatimaye walijihusisha na harakati za kudai uhuru.


                                                  61




                                                                                        03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   61                                         03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   61
   64   65   66   67   68   69   70   71   72   73   74