Page 64 - Historia_Maadili
P. 64

Harakati za kudai
               Sura ya Nne
                                                 uhuru wa Tanganyika


                                                         na Zanzibar
        FOR ONLINE READING ONLY


                     Utangulizi



              Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ziliendana na juhudi
              mbalimbali za kisiasa na kijamii zilizolenga kukomesha utawala wa kikoloni.
              Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya uhuru na harakati za kudai uhuru,
              pamoja na misingi na mbinu zilizotumika katika kupigania uhuru wa Tanganyika
              na Zanzibar. Pia, utajifunza mchango wa harakati hizo katika kuupinga utawala
              wa kikoloni, kuyatunza maadili ya Kitanzania na kuujenga uzalendo. Umahiri
              utakaoupata utakuwezesha kuthamini juhudi za wapigania uhuru wa Tanganyika
              na Zanzibar na pia kuuheshimu na kuuenzi uhuru wetu.




                     Fikiri



              Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.




          Dhana ya uhuru na harakati za kudai uhuru
          Neno “uhuru” linaweza kufafanuliwa  kwa namna mbalimbali. Uhuru ni hali ya mtu
          au nchi kuamua na kufanya mambo yake bila kuingiliwa na mtu au taifa lolote, iwe
          kiuchumi, kisiasa, kijamii au kiutamaduni. Katika muktadha huu, uhuru ni hali ya nchi
          kujikomboa kutoka kwenye ukoloni wa mataifa ya kibepari. Harakati za kudai uhuru
          wa Tanganyika na Zanzibar ni mchakato au juhudi za watu wa nchi hizo kutafuta
          uhuru kutoka kwa serikali za kikoloni. Pia, ni hatua zilizochukuliwa na wananchi wa
          Tanganyika na Zanzibar hadi kufanikisha kupata uhuru wao.
          Tanganyika ilitawaliwa na wakoloni wa Kijerumani kuanzia mwaka 1885 hadi 1918.
          Baada ya Vita ya Kwanza vya Dunia, Tanganyika ilitawaliwa na Waingereza hadi
          ilipopata uhuru wake tarehe 9 Desemba, 1961. Zanzibar ilikuwa chini ya utawala
          wa Kisultani kutoka Oman kuanzia mwaka 1840 hadi 1890, kisha ikatawaliwa
          na Waingereza kuanzia mwaka 1890 hadi 1963. Baada ya harakati za kutafuta
          uhuru,Waingereza walikabidhi uhuru wa Zanzibar kwa vyama vya ZNP na ZPPP


                                                  56




                                                                                        03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   56                                         03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   56
   59   60   61   62   63   64   65   66   67   68   69