Page 60 - Historia_Maadili
P. 60

wavamizi kama Wajerumani baadae. Lakini baadae  mpango wao ulishindwa na wao
          kujikuta wakitawaliwa kirahisi zaidi. Mfano wa jamii hizi za Kitanzania ni kama vile
          Wachaga. Ambao chini ya Mangi Mandara waliungana na Wajerumani ili kumshinda
          Mangi Sina; Mangi Marealle aliungana na Wajerumani ili kumshinda Mangi Meli;
          Wasangu na Wabena chini ya Mtwa Merere na Mbeyela mtawalia waliungana na
          Wajerumani dhidi ya Wahehe chini ya Mtwa Mkwawa na jamii zingine nyingi.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Ukweli ni kwamba jamii hizi zote zilishindwa kupata walichokitarajia  na mwisho
          kutawaliwa kirahisi sana na Wajerumani. Hivyo, usaliti wao dhidi ya watawala wa
          jamii za Kitanzania kwa kuungana na wakoloni Wakijerumani ulikuwa ni fedheha
          kwao kwani haukuwa na manufaa yoyote.


          Kwa njia ya kusalimu amri

          Kuna baadhi ya jamii za Kitanzania ambazo hazikupenda kutawaliwa na wakoloni
          lakini zilijiona hazina uwezo wa kuweza kukabiliana na Wajerumani kivita. Nyingi
          ya jamii hizi ni zile zilizokuwa zimeathirika na baa la njaa au magonjwa, ukosefu
          wa dola zenye nguvu mazingira magumu ya kivita na sifa nyingine kama hizo. Kwa
          mfano, jamii ya Kimasai hapa nchini ilisalimu amri kwa Wajerumani kufuatia kupatwa
          na majanga ya magonjwa ya Wanyama miaka ya 1870s na 1880s na mazingira yake
          kutokuwa mazuri kwa vita.

                              Zoezi la           3.3



            1.  Fafanua namna jamii za Watanzania na viongozi wao walivyoupinga utawala
               wa Wajerumani.
            2.  Eleza mbinu zinazoweza kutumiwa na jamii za sasa za Kitanzania kulinda
               rasilimali, utamaduni na maadili ya jamii zao.

            3.  Eleza kwa nini vita ya Maji Maji hujulikana kama vita kubwa Tanzania.



          Changamoto zilizokabili mapambano dhidi ya uvamizi wa kikoloni
          Wananchi walijaribu kupambana na kupinga ukoloni, lakini wakoloni waliwazidi
          nguvu na kuwashinda. Zipo sababu nyingi zilizowafanya wananchi kushindwa katika
          mapambano hayo. Miongoni mwa sababu hizo ni kama zinavyoelezwa katika sehemu
          zinazofuata.

          Ukosefu wa umoja miongoni mwa jamii za Kitanzania
          Kama ilivyoonekana, mapambano dhidi ya ukoloni yalifanywa kati ya wakoloni na
          jamii moja moja za Kitanzania. Hii inamaanisha kuwa, katika kipindi cha ukoloni,
          jamii za Kitanzania zilishindwa kwa sababu zilikosa umoja na hazikushirikiana
          kupambana na wakoloni. Kwa mfano, hata katika vita ya Maji Maji, makabila
          hayakuungana yote kwa pamoja kila kabila lilipigana kivyake katika eneo lake.


                                                  52




                                                                                        03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   52                                         03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   52
   55   56   57   58   59   60   61   62   63   64   65