Page 56 - Historia_Maadili
P. 56

FOR ONLINE READING ONLY














          Kielelezo 3.2: Mtwa Mkwawa             Kielelezo 3.3: Mnara wa kumbukumbu
                                                  walipouwawa askari wa Kijerumani

          Licha ya kushindwa mwaka 1891, Wajerumani waliendelea kujiimarisha kivita
          kwa kuanzisha vikosi vya kijeshi katika maeneo ya Kilosa na Kisaki. Baada ya

          kujiimarisha, Wajerumani walituma wajumbe kwa Mtwa Mkwawa wakimtaka
          aitambue serikali ya Wajerumani, alipe gharama za vita, aache kuvamia misafara ya
          kibiashara katika maeneo jirani na utawala wake, asalimishe silaha zilizotekwa na
          aruhusu wafanyabiashara na wamisionari kutumia eneo lililokuwa chini ya utawala
          wake. Mkwawa alikataa mapendekezo yote hayo, akipinga ukatili, unyonyaji na
          unyanyasaji uliokuwa unafanywa na Wajerumani.

          Mwaka 1894, Wajerumani chini ya Kamanda Tom Prince walivamia ngome ya
          Wahehe huko Kalenga. Mkwawa alikimbilia mafichoni na kuendelea na vita vya

          msituni. Mwaka 1898, Mtwa Mkwawa aliamua kujiua badala ya kukamatwa na
          Wajerumani. Kifo cha namna hii kilikuwa ushujaa wa aina yake, kwani Mkwawa
          aliona ni fedheha kwa shujaa kukamatwa, kunyanyaswa na kuuawa kikatili kwa
          kunyongwa na wavamizi.

          Mapambano ya Wayao: Mapambano ya kupinga uvamizi wa Wajerumani upande
          wa kabila la Wayao yaliongozwa na kiongozi wao jasiri na shupavu, Mwene
          Machemba. Mwene Machemba alishinda karibu mapigano yote aliyoyaongoza dhidi

          ya Wajerumani. Ushindi huu ulitokana na ukweli kwamba Mwene Machemba alikuwa
          kiongozi hodari, shupavu na mwenye kupenda kutetea maadili na uhuru wa watu
          wake. Kwa mfano, katika barua aliyowaandikia Wajerumani, Mwene Machemba


                                                  48




                                                                                        03/10/2024   18:15:13
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   48                                         03/10/2024   18:15:13
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   48
   51   52   53   54   55   56   57   58   59   60   61