Page 53 - Historia_Maadili
P. 53

Zoezi la          3.2


             1.  Je, ni sababu gani ziliwafanya jamii za Kitanzania kupinga utawala wa
                 kikoloni?

             2.  Eleza mbinu ambazo jamii za sasa za Kitanzania  zinaweza kutumia
        FOR ONLINE READING ONLY
                 kulinda rasilimali, utamaduni na maadili ya jamii zao.

             3.  Jadili namna maadili ya Watanzania yaliyokiukwa kutokana na uvamizi
                 wa kikoloni.
             4.  Fafanua athari za kiuchumi kwa jamii za Kitanzania zilizosababishwa na
                 utawala wa kikoloni.



          Upinzani dhidi ya uvamizi wa kikokoni katika jamii za Kitanzania
          Karibu jamii zote za Kitanzania ziliupinga uvamizi wa kikoloni kwa sababu hakuna
          jamii iliyopenda kuupoteza uhuru na utamaduni wake kwa wageni. Jinsi jamii hizi
          zilivyoupinga uvamizi huo, au njia gani walizozitumia zilitegemea uwezo wa kivita,
          kiuchumi, mazingira na uongozi bora na imara. Kwa hiyo, kuna jamii zilizoupinga
          ukoloni kwa kupigana vita, zingine kwa kujisalimisha na nyingine kwa kuungana
          na wavamizi.


          Njia ya kupambana kwa vita
          Njia ya vita ilikuwa maarufu zaidi kati ya jamii za Kitanzania, kwani jamii nyingi
          hazikuwa tayari kuupoteza uhuru wao na hivyo ziliupinga waziwazi uvamizi huo
          kwa kutumia vita. Jamii hizi nyingi zilikuwa na uongozi shupavu, zilimiliki silaha,
          zilikuwa na uwezo wa kiuchumi na nyingi pia zilikuwa chini ya dola zenye nguvu.
          Mapambano dhidi ya uvamizi yalihusisha jamii moja moja au jamii nyingi kwa
          pamoja. Kwa mfano, mapambano ya mwanzo dhidi ya uvamizi wa kikoloni na maadili
          yake yalihusisha jamii moja moja na siyo makabila mengi au nchi nzima.


          Mapambano ya Wanyamwezi: Harakati za kuupinga uvamizi wa kikoloni magharibi
          mwa Afrika Mashariki ya Kijerumani, ziliongozwa na Mtemi wa Wanyamwezi
          aliyejulikana kama Isike au Mwana Kiyungi kuanzia mwaka 1886 hadi 1891. Mtemi
          Isike alipinga vikali uvamizi wa Wajerumani katika himaya yake baada ya maeneo
          yake ya kiutawala kuporwa. Pia, alitetea masilahi ya biashara iliyokuwa ikifanyika
          miongoni mwa jamii ya Wanyamwezi huko Tabora. Mtemi Isike alikusanya ushuru
          kutoka kwa wafanyabiashara wa Kiarabu waliokuwa wakipita katika himaya yake
          kuelekea Ujiji mpaka Katanga (sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo), Burundi
          na wengine kaskazini kuelekea kanda ya Ziwa Viktoria hadi ufalme wa Buganda na
          Bunyoro.


                                                  45




                                                                                        03/10/2024   18:15:12
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   45
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   45                                         03/10/2024   18:15:12
   48   49   50   51   52   53   54   55   56   57   58