Page 50 - Historia_Maadili
P. 50

Sura ya Tatu                     Mapambano ya awali dhidi

                                                  ya uvamizi wa kikoloni


        FOR ONLINE READING ONLY

                   Utangulizi



            Jamii za Kitanzania zilitumia mbinu na njia mbalimbali kuukataa na kuupinga
            uvamizi wa kikoloni. Katika sura hii, utajifunza kuhusu dhana ya uvamizi wa
            kikoloni na sababu za kupinga uvamizi wa kikoloni. Pia, utajifunza mbinu na
            njia zilizotumika katika kuupinga uvamizi wa kikoloni. Umahiri utakaoujenga
            utakusaidia kuenzi, kuthamini na kuendeleza harakati za ukombozi dhidi ya
            unyonyaji na ukandamizaji wa aina mbalimbali katika jamii.




                   Fikiri



             Mapambano ya jamii za Kitanzania dhidi ya uvamizi wa kikoloni.





          Dhana ya uvamizi wa kikoloni
          Uvamizi wa kikoloni ni kitendo cha nchi moja kuingia katika nchi nyingine kwa lengo
          la kuanzisha utawala wake kisiasa, kiuchumi na kijamii. Mara nyingi, uvamizi huu
          hutekelezwa kwa kutumia nguvu za kijeshi. Uanzishwaji wa utawala wa kikoloni
          hutegemea kushindwa kwa nchi inayovamiwa kujilinda au kuzuia uvamizi huo.
          Uvamizi wa kikoloni nchini Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) ulipingwa vikali
          kwa sababu jamii za Kitanzania zilifahamu kwamba kuruhusu wakoloni kuvamia
          kungesababisha kupoteza uhuru wao.
          Kwa sababu za kizalendo na kupenda jamii zao, viongozi wengi wa jamii za Kitanzania
          waliongoza mapambano dhidi ya uvamizi huo tangu miaka ya 1880 na mapambano
          hayo yaliendelea hata baada ya ukoloni kuanzishwa nchini Tanganyika. Wananchi
          walipinga na kuonesha wazi hisia zao za kutokubali dhuluma na unyanyasaji kutoka
          kwa wakoloni, hali iliyojitokeza karibu katika kila sehemu ya Tanzania. Mapambano
          ya awali dhidi ya wakoloni yalihusisha jamii moja moja, jambo ambalo linamaanisha
          kuwa, hatua za mwanzo za kuupinga uvamizi wa kikoloni hazikuhusisha nguvu za
          pamoja za jamii mbalimbali za Kitanzania au taifa moja la Tanzania.


                                                  42




                                                                                        03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   42
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   42                                         03/10/2024   18:15:11
   45   46   47   48   49   50   51   52   53   54   55