Page 54 - Historia_Maadili
P. 54
Ili kulinda uhuru na maadili ya jamii ya Wanyamwezi, Mtemi Isike aliwaongoza kwa
ushupavu askari wake kupambana na majeshi ya Wajerumani. Zaidi ya askari 1000
wa jeshi la Wajerumani walipambana vikali na askari wa Isike. Hata hivyo, ngome ya
Mtemi Isike ilivunjwa na majeshi ya kivamizi ya Wajerumani. Isike alipoelemewa,
aliona ni bora ajiue kuliko kukamatwa na Wajerumani, hivyo alijilipua kwa baruti
pamoja na familia yake mnamo mwaka 1893. Hii inaonesha kuwa Mtemi Isike
FOR ONLINE READING ONLY
alikuwa mzalendo wa kweli aliyekuwa tayari kufa kwa ajili ya nchi yake na hakuwa
tayari kunyanyaswa na wavamizi wa kikoloni.
Mapambano ya jamii za watu wa pwani: Mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa
Kijerumani katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki ya Kijerumani (sasa
Tanzania) yaliongozwa na wafanyabiashara mashuhuri Abushiri bin Salim al-Harthi
wa Pangani na Bwana Heri bin Juma wa Uzigua. Viongozi hawa waliongoza
mapambano dhidi ya sera za unyonyaji za Wajerumani, ambazo zilivuruga na kutishia
masilahi ya biashara katika ukanda wa pwani na pia kupora uhuru wao.
Mwaka 1889, Abushiri bin Salim aliwaongoza wananchi wa pwani katika maeneo
ya Pangani kupigana na Wajerumani na
kufanikiwa kuwaondoa katika baadhi ya
maeneo ya pwani. Kutokana na upinzani
mkali alioutoa kwa majeshi ya Kijerumani,
Wajerumani waliomba msaada kutoka kwa
majeshi ya Uingereza. Muungano huu
ulisababisha Abushiri kukimbia kwa sababu
za kiusalama. Kwa kutumia njia ya kugawa
umoja miongoni mwa jamii za Kitanzania,
Wajerumani walifanikiwa kumkamata
Abushiri bin Salim al-Harthi baada ya
kusalitiwa na Chifu Magaya wa Usagara.
Mwaka 1889, Abushiri bin Salim al-Harthi
aliuawa kikatili kwa kunyongwa hadharani
na Wajerumani huko Bagamoyo. Kielelezo Kielelezo 3.1: Abushiri bin Salim
3.1 kinaonesha Abushiri bin Salim.
Bwana Heri bin Juma aliwaongoza Wazigua wa maeneo ya Saadani dhidi ya uvamizi
wa Wajerumani. Ingawa baadaye alishindwa, aliendesha mapambano makali ambayo
yalionesha jinsi wananchi walivyokuwa hawako tayari kunyanyaswa na kunyonywa
na Wajerumani. Wakati huo huo, mapambano dhidi ya Wajerumani katika maeneo
ya Kilwa Kivinje yaliongozwa na Hassan bin Omari Makunganya mwaka 1894.
Kama ilivyokuwa kwa mashujaa wengine, Makunganya alipambana vikali sana
katika maeneo yake. Hata hivyo, baadaye alikamatwa na kunyongwa na Wajerumani
huko Kivinje kwenye mwembe ambao mpaka sasa unajulikana kama “Mwembe
Kunyonga.”
46
03/10/2024 18:15:12
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 46 03/10/2024 18:15:12
HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd 46

