Page 52 - Historia_Maadili
P. 52

Sababu za kuupinga uvamizi wa kikoloni na maadili yake
          Utawala wa kikoloni nchini Tanzania ulisababisha kupotea kwa uhuru, kudunishwa
          na kuharibiwa kwa maadili ya jamii. Wakoloni walidhihaki mila na desturi ambazo
          zilikuwa msingi wa maadili ya jamii. Hali hii iliwachochea wananchi, chini ya uongozi
          wa viongozi wao hodari na shupavu wa jadi, kuupinga utawala wa kigeni ili kulinda
          uhuru, utamaduni na maadili yao.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Aidha, wananchi walinyonywa kwa kulazimishwa kufanya kazi za vibarua na kulipwa
          ujira mdogo katika mashamba ya mkonge, pamba, chai, tumbaku na pareto. Wakulima,
          wakiwa chini ya usimamizi mkali wa majumbe na wanyapara, walidhalilishwa kwa
          kuchapwa viboko. Pia, wananchi walilazimishwa kulima mazao ya biashara kama
          pamba, kahawa na chai kwa faida ya wakoloni na mabepari wa Ulaya Magharibi,
          ambapo mazao hayo yaliuzwa kwa bei ndogo.

          Zaidi ya hayo, mfumo mpya wa kodi ulioanzishwa na wakoloni uliwalazimisha
          wananchi kulipa kodi ya kichwa na kodi nyingine kwa pesa tasilimu. Jambo hili
          liliwakera sana kwa kuwa hawakuwa na pesa, hivyo walilazimika kuuza mifugo yao,
          kufanya kazi za vibarua kwa wakoloni na walowezi au kulima mazao ya biashara ili
          kupata pesa za kulipa kodi.
          Wakoloni walitumia adhabu za kikatili kama kuwanyonga viongozi wa jamii
          za Kitanzania waliopinga utawala na maadili yao. Wananchi pia waliteswa na
          kudhalilishwa hadharani kwa kuchapwa viboko waliposhindwa kulipa kodi au
          walipotenda makosa mengine dhidi ya utawala wa kikoloni, jambo lililoshusha
          heshima, ushujaa na utu wao ambao ulikuwa umejengwa kwa muda mrefu na jamii
          zao za asili.

          Aidha, ardhi yenye rutuba iliporwa na wakoloni kwa ajili ya kilimo cha mazao ya
          biashara, hali iliyowafanya wananchi washindwe kukidhi mahitaji yao ya chakula
          kutokana na kuwa na mashamba madogo yasiyo na rutuba ya kutosha. Hatimaye,
          wananchi walinyang’anywa udhibiti wa maeneo yao ya biashara kwa mfano, Wahehe
          walipambana na Wajerumani walipojaribu kuimarisha na kupanua mipaka yao ya
          biashara, jambo lililosababisha chuki na mapambano.





           Kazi ya kufanya 3.3


            Fanya utafiti mdogo, kisha andika taarifa kuhusu jinsi uvamizi wa kikoloni
            ulivyosababisha mmomonyoko wa maadili katika jamii za Kitanzania.







                                                  44




                                                                                        03/10/2024   18:15:12
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   44                                         03/10/2024   18:15:12
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   44
   47   48   49   50   51   52   53   54   55   56   57