Page 57 - Historia_Maadili
P. 57

alisema: “Nimesikiliza maneno yenu, lakini sijaona
          sababu ya kuwatii. Niko tayari kufa…, sisemi mnitii
          mimi kwa kuwa nyie ni watu huru kama mimi.”
          Maneno haya yanaonesha jinsi alivyosimamia utu
          na uhuru wa watu wake kwa ujasiri mkubwa.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Hata hivyo, Mwene Machemba alikimbilia

          Msumbiji baada ya kupambana vikali na majeshi
          ya Wajerumani, ambapo Wayao walizidiwa nguvu
          na kushindwa vita. Kielelezo 3.4 kinaonesha picha
          ya Mwene Machemba.                               Kielelezo 3.4: Mwene Machemba


          Mapambano ya Wachaga: Mapambano dhidi ya uvamizi wa Wajerumani katika jamii
          ya Wachaga yaliongozwa na viongozi wa Kibosho na Moshi. Kwa upande wa Kibosho,
          wakiwa chini ya uongozi wa Mangi Sina, walipinga kitendo cha Wajerumani kuingilia
          mgogoro uliokuwepo miongoni mwa   watawala wa Kibosho, Moshi na Marangu.
          Kitendo hicho kilimuudhi Mangi Sina, kwani kilionekana kuwa na nia ya kuwagawa.
          Kwa hasira, Mangi Sina aliichana bendera ya Wajerumani, kitendo ambacho kilikuwa
          ishara ya kuupinga ukatili na unyanyasaji uliokuwa unafanywa na Wajerumani
          Uchagani. Kitendo hicho kiliwakasirisha Wajerumani, ambao walituma majeshi ya
          kukodi ya Wanubi kutoka Sudani ili kupambana naye. Hata hivyo, baada ya kuzidiwa
          nguvu na majeshi ya Wajerumani, Mangi Sina alilazimika kutoroka.

          Vilevile, Mangi Meli aliongoza mapambano dhidi
          ya Wajerumani huko Moshi, akipinga ukatili na
          mfumo wa unyanyasaji na unyonyaji wa wakoloni.
          Katika mapambano hayo, kamanda wa jeshi la
          Wajerumani, Von Bulow, aliuawa. Kwa kulipiza
          kisasi, Wajerumani walimshambulia Mangi Meli,
          wakamkamata na baadaye wakamnyonga kwa ukatili
          kijijini kwake. Kielelezo 3.5 kinaonesha picha ya
          Mangi Meli.
                                                               Kielelezo 3.5:  Mangi Meli
          Vita vya Liti Kidanka dhidi ya Wajerumani (1908-1910): Wajerumani walifika Singida
          mnamo mwaka 1901. Wajerumani walikabiliana na upinzani mkali kutoka kwa
          Wanyaturu, walioongozwa na mwanamke shupavu, Liti Kidanka, kupinga uvamizi
          huo. Liti Kidanka hakutaka Wajerumani watawale eneo ambalo sasa ni Mji wa Singida.
          Hivyo, aliongoza mapambano makali dhidi ya askari wa Kijerumani walioongozwa
          na Kapteni Eberhard von Sick.


                                                  49




                                                                                        03/10/2024   18:15:13
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   49                                         03/10/2024   18:15:13
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   49
   52   53   54   55   56   57   58   59   60   61   62