Page 59 - Historia_Maadili
P. 59

FOR ONLINE READING ONLY





































                           Kielelezo 3.7: Jamii zilizopinga utawala wa Wajerumani


           Kazi ya kufanya 3.5


            Kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya taarifa ikiwemo mitandao andika  nukuu
            ya Mwene Machemba kwenye barua aliyowaandikia Wajerumani, kisha eleza
            jinsi alivyopinga uvamizi kwa nguvu zake zote.


          Kwa njia ya kuungana

          Kuna jamii za Kitanzania zilijua nguvu ya kijeshi ya Wajerumani na hawakuwa tayari
          kupambana na kuupinga uvamizi wao moja kwa moja. Lakini waliungana ili kuweza
          kuwashinda maadui wao. Hii ilitokana na imani kwamba, baada ya kuwashinda
          maadui wao wa muda mrefu wangebaki kuwa na nguvu zaidi na kujiimarisha. Pia,
          kuungana huku walikusudia kupata misaada ya silaha na vifaa vingine kutoka kwa
          Wajerumani. Silaha na vifaa hivyo vingewafanya kuwa imara zaidi hata kuwashinda

                                                  51




                                                                                        03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   51
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   51                                         03/10/2024   18:15:14
   54   55   56   57   58   59   60   61   62   63   64