Page 63 - Historia_Maadili
P. 63

Hofu miongoni mwa Watanzania: Vita vilisababisha kujengeka kwa hofu miongoni
          mwa Watanzania. Kutokana na kushindwa kwa mapambano, watu wengi walipata
          hofu ya kupigana tena na Wazungu.

          Mateso na vifo vingi: Vita vya kupinga uvamizi wa wakoloni vilisababisha maelfu ya
          vifo katika mapambano, kukamatwa kwa mateka, kunyongwa na vifo vilivyotokana
          na njaa wakati na baada ya vita. Vilevile, vita viliathiri uzalishaji wa mazao ya
        FOR ONLINE READING ONLY
          biashara kama vile pamba, mkonge na mpira na pia iligharimu serikali ya kikoloni
          kiasi kikubwa cha fedha kugharamia vita. Kwa sababu hiyo, Wajerumani walilazimika
          kufanya mabadiliko katika sera zao za utawala na uchumi ili kupunguza migogoro
          na wananchi.
          Mwamko mpya wa harakati za uhuru: Ingawa jamii za Kitanzania zilishindwa
          katika mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa kikoloni, mapambano hayo yaliacha
          alama muhimu katika historia. Jamii hizi zilionesha ujasiri na dhamira ya kweli ya
          kupinga ukandamizaji wa kigeni. Hali hii ilichochea mwamko mpya wa wapigania
          uhuru wa baadaye, ambao walijifunza mengi kutoka kwa harakati hizo za kitaifa za
          kudai uhuru.

          Kumbukumbu muhimu katika historia ya Tanzania: Hapana shaka kwamba vita
          vya kupinga ukoloni ni kumbukumbu muhimu katika historia ya Tanzania inayostahili
          kuheshimiwa na yeyote anayethamini utu, uhuru, haki, heshima na usawa. Vita
          hivyo ni kielelezo halisi cha Watanzania kukataa utawala wa kikoloni. Wajerumani
          walijifunza kwamba mababu na mabibi zetu walikuwa tayari kuutetea na kuulinda
          uhuru na rasilimali zao. Miaka mingi imepita tangu vita hivyo kutokea na kila
          Mtanzania anapaswa kujiuliza ni mafundisho yapi anaweza kujifunza kutokana na
          matukio hayo. Je, bado tunao ule moyo wa ushujaa, uzalendo, heshima na usawa
          kama ilivyokuwa enzi za mababu na mabibi zetu?

                                   Zoezi la marudio

            1.  Tofautisha kati ya maadili ya kikoloni na maadili ya jamii za Kitanzania
                wakati ukoloni unaingia.
            2.  Eleza sababu za kushindwa kwa mapambano ya awali ya jamii za Kitanzania
                dhidi ya uvamivi wa kikoloni.

            3.  Eleza jinsi viongozi wa sasa wanapaswa kutetea masilahi ya wananchi kwa
                ujasiri na uzalendo.

            4.  Bainisha  vitendo  vya kijasiri  vilivyooneshwa  na viongozi  wa jamii  za
                Kitanzania waliongoza mapambano ya awali dhidi ya uvamizi wa kikoloni.
            5.  Je,  unafikiri  ni  namna  gani  mbinu  ya  jadi  ya  kivita  iliyotumiwa  na
                Kinjeketile ilisaidia katika kupinga uvamizi wa Wajerumani?

            6.  Ni funzo gani viongozi wa sasa wanaweza kujifunza kutoka kwa jamii za
                Kitanzania zilizopinga uvamizi wa Wajerumani?

                                                  55




                                                                                        03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   55                                         03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   55
   58   59   60   61   62   63   64   65   66   67   68