Page 66 - Historia_Maadili
P. 66

Watanzania walilazimishwa kujenga miundombinu mbalimbali. Kwa mfano, watu
          walijenga reli ya kati na Tanga, 1893-1911, kwa lazima na kuchapwa viboko pale
          walipogoma kufanya kazi. Watu walilazimika kufanya kazi hata pale walipokuwa
          wamechoka. Hali hii iliwakasirisha sana Watanzania.

          Kudhihakiwa kwa mila na desturi za Watanzania: Wakoloni kupitia Wamisionari
        FOR ONLINE READING ONLY
          walipiga marufuku mila na desturi za Kiafrika. Kwa mfano, majina ya Kiafrika
          yalionekana ni ya “kishenzi” na vilevile dini za jadi zilionekana ni za “kishenzi”.
          Baadhi ya vyakula, nguo, lugha na sanaa vilipigwa marufuku. Badala yake walitilia
          mkazo matumizi ya utamaduni wa kigeni. Dini za Ukristo na Uislamu zikawa ni
          alama ya ustaarabu kwa Waafrika waliozifuata imani hizi. Hali hii iliwakasirisha
          wanajamii na hivyo hawakuwa tayari kuona mila na desturi zao zikidharaulika. Kwa
          mfano, moja ya sababu za kuibuka kwa vita vya Maji Maji katika eneo la Songea
          ni kudhihakiwa na kuchomwa moto kwa eneo la ibada za jadi za jamii ya Wangoni
          huko Maposeni karibu na Peramiho. Kitendo hicho kilisababisha kuuawa kwa padri
          mwenye asili ya Ujerumani aliyeitwa Franciscus Leuthner pamoja na kuvunjwa kwa
          kanisa katika eneo la Peramiho tarehe 10 Septemba mwaka 1905.

          Kuongozwa na wakoloni: Wakoloni walitaka kutawala Tanganyika na Zanzibar
          kwa muda mrefu. Hivyo, mifumo ya kiutawala haikutoa nafasi kwa Waafrika
          kuendelea na utamaduni wao wa kuongozwa na viongozi wao wa jadi. Utawala wa
          kikoloni ulidhihirisha kupotea kwa uhuru wa Watanzania kwani hawakuwa huru.
          Hata pale viongozi wao wa jadi walipokuwa wakitawala kupitia mfumo wa uwakala.
          Hata hivyo, uamuzi wote ulitolewa na wakoloni kupitia gavana au wasaidizi wake
          kama wakuu wa mikoa (provincial commissioners) au wakuu wa wilaya (district
          commissioners). Mambo haya yaliwaudhi sana wananchi na kuamua kutafuta
          uhuru wao uliopotea. Mbaya zaidi hata pale wakoloni walipotakiwa kuwaandaa
          Watanganyika na Wazanzibari kujitawala, wao waliendelea kuwatawala kwa manufaa
          yao. Kwa mfano, Umoja wa Mataifa uliwapa Waingereza jukumu la kuisimamia na
          kuiandaa Tanganyika kujitawala baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, badala
          yake hawakuwa na mpango wa kuondoka na kutoa uhuru kwa Watanganyika. Hivyo,
          waliendelea kujiimarisha kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni ili kuendelea kuitawala
          Tanganyika kwa manufaa ya taifa lao la Uingereza. Hivyo, hali hii iliwakasirisha
          Watanganyika na kuamua kuanzisha harakati za kudai uhuru.



           Kazi ya kufanya 4.1


            Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mitandao ili kubainisha misingi
            mingine ya kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.






                                                  58




                                                                                        03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   58                                         03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   58
   61   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71