Page 67 - Historia_Maadili
P. 67

Zoezi la          4.1

            1.  Kwa kutumia mifano, eleza maana ya harakati za kupigania uhuru.

            2.  Kwa nini  wananchi  wa Tanganyika  na  Zanzibar  walianzisha  harakati  za
               kudai uhuru?
        FOR ONLINE READING ONLY
            3.  Eleza kwa nini wakoloni walitumia sera za unyonyaji na ubaguzi wakati
               wanatawala Tanganyika.
            4.  Tofautisha maadili ya kikoloni na yale ya jamii za Kitanzania wakati ukoloni
               unaingia Tanganyika.

            5.  Je, ni athari gani zilizotokea kutokana na kudharauliwa kwa mila na desturi
               za jamii za Kitanzania?


          Mbinu zilizotumika kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

          Kuna vipindi viwili muhimu vya harakati za wananchi katika kudai uhuru wa
          Tanganyika na Zanzibar. Kipindi cha kwanza kilikuwa kati ya mwaka 1900 hadi
          1944. Katika kipindi hicho, harakati ziliendeshwa na vikundi na vyama vya kijamii
          na kidini (hasa kwa upande wa Tanganyika) katika maeneo machache tu. Kipindi
          cha pili cha harakati hizi kilikuwa kati ya mwaka 1945 na 1964, ambapo harakati za
          kudai uhuru zilikuwa na nguvu zaidi zikiendeshwa na vyama vya siasa. Katika kipindi
          hiki, harakati hizo zilisambaa nchi nzima kutokana na mabadiliko yaliyotokana na
          mchango wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1939 – 1945).

          Harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar zilitumia mbinu mbalimbali,
          ikiwa ni pamoja na kuanzisha jumuiya, vyama na taasisi za kijamii za Waafrika.
          Malengo ya kuanzishwa kwa jumuiya, vyama na taasisi hizo yalikuwa ni kutetea na
          kudai haki za wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara. Kadiri muda ulivyoendelea,
          jumuiya, vyama na taasisi hizo zilijihusisha na siasa na kuchangia sana katika harakati
          za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.

          Vyama vya ushirika na wakulima

          Chama cha ushirika ni muungano wa watu waliokubaliana kuendesha shughuli zao
          za kiuchumi kwa pamoja ili kuinua hali zao za maisha. Shughuli hizi ni kama vile
          kutafuta mahitaji yao ya chakula, elimu, uuzaji wa mazao yao na shughuli nyingine
          za uchumi zinazoweza kuendeshwa kwa pamoja. Hata hivyo, jambo la muhimu
          ni kuhakikisha kuwa watu hao wana mahitaji yanayofanana ya kupata huduma ya
          shughuli yoyote ya kiuchumi iliyowafanya waanzishe chama.

          Vyama vya wakulima vilianzishwa na wakulima wenyewe katika maeneo ambapo
          mazao ya biashara yalilimwa. Vyama hivi vilijulikana kama vyama vya ushirika katika
          sehemu mbalimbali za Tanganyika na Zanzibar. Baadhi ya malengo ya kuanzishwa
          kwa vyama hivi yalikuwa ni pamoja na kudai bei nzuri ya mazao yao, kupata

                                                  59




                                                                                        03/10/2024   18:15:14
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   59
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   59                                         03/10/2024   18:15:14
   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71   72