Page 70 - Historia_Maadili
P. 70

Kazi ya kufanya 4.2


            Chagua chama kimojawapo cha ushirika au wafanyakazi kilichoshiriki harakati
            za kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, kisha soma matini mbalimbali kupitia
        FOR ONLINE READING ONLY
            mtandao kuhusu chama hicho na andika maelezo yenye kurasa 2 kuhusu historia
            na mchango wake katika harakati za kudai uhuru




          Vyama vya wafanyabiashara

          Vyama vya wafanyabiashara wa Kiafrika vilianzishwa nchini Tanganyika ili kuyalinda
          na kuyatetea masilahi ya wafanyabiashara wa Kiafrika dhidi ya wafanyabiashara wa

          kigeni. Baadhi ya madai yao yalijumuisha kupinga ubaguzi na unyanyasaji katika
          masoko, kupinga kodi kubwa iliyokuwa ikitozwa na kuboresha mazingira ya kufanyia
          biashara. Mfano wa vyama hivi ni African Commercial Association kilichoanzishwa

          mwaka 1934 chini ya Erica Fiah. Hata hivyo,  Fiah alikibadilisha chama hiki na
          kukifanya Tanganyika African Welfare and Commercial Association mwaka 1936,
          kisha kuanzishwa tena kama African Retail Traders’ Association mwaka 1937.

          Kwa upande wa Zanzibar, kulikuwa na jumuiya mbalimbali za Wahindi, Waarabu na

          Waafrika zilizoundwa ili kutetea masilahi yao ya kifedha na kibiashara. Mfano wa
          jumuiya hizo ni Jumuiya ya Wahindi iliyoundwa mwaka 1910, ambayo ilianzishwa
          ili kupambana na Waarabu waliokuwa wanadaiwa fedha nyingi na Wahindi baada ya
          kufilisika kutokana na kufutwa kwa biashara ya utumwa Zanzibar. Pamoja na madai
          haya, kulikuwa na harakati za chini kwa chini kuhusu masuala ya kisiasa.


          Vyama vya kijamii viliendelea kukua mwaka hadi mwaka nchini Tanganyika na
          Zanzibar na vilianzishwa vyama vyenye lengo la kuwaunganisha watu wa maeneo na
          sekta mbalimbali. Mfano wa vyama hivi ni Tanganyika African Association (TAA),

          kilichoanzishwa mjini Dar es Salaam mwaka 1929. Chama cha TAA kiliundwa
          na watumishi wa serikali na baadaye kikazaa chama cha siasa kiitwacho TANU.
          Rais wake wa kwanza alikuwa Cecil Matola na katibu wake alikuwa Abdulwahid
          Kleist Sykes. Kufikia mwaka 1948, TAA kilikuwa na matawi makuu Dar es Salaam

          na Dodoma. Zanzibar kulikuwa na African Association na Shirazi Association.
          Jumuiya hizi mbili zilizoundwa Zanzibar zilikuja kuungana na kuunda chama cha




                                                  62




                                                                                        03/10/2024   18:15:15
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   62
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   62                                         03/10/2024   18:15:15
   65   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75