Page 74 - Historia_Maadili
P. 74

na michezo kama vile kikundi cha taarabu cha Jipisheni. Kikundi hicho baadaye
          kilipewa jina la Egyptian Music Club. Kikundi kingine cha taarabu kilikuwa ni
          Al-Watan. Pamoja na taarabu kulikuwa vikundi vya lelemama ambavyo vilikuwa

          na udugu na vikundi vya taarabu vya Al-Watan au Egyptian. Vikundi vyote hivi
          vilitoa mchango mkubwa sana katika kuhamasisha watu kuiunga mkono TANU.
        FOR ONLINE READING ONLY
          Waliounganisha na kuviongoza vyama hivi vya wanawake na harakati za kudai uhuru
          walikuwa Bibi Titi Mohamed na Bibi Hawa binti Maftah. Kielelezo 4.5 kinaonesha
          picha ya Bibi Titi Mohamed akiwa jukwaani.

          Kulikuwa pia na vyama vya wanawake kama Nujum ul Azhar na Egyptian Club
          vilivyokuwepo mjini Tabora. Vyama hivi viliongozwa na wanawake kama Nyange

          binti Chande na Zarura binti Abdulrahman na vilichangia sana kuipa TANU nguvu
          katika Jimbo la Magharibi. Muziki na ujumbe uliokuwa katika nyimbo zilizotungwa
          maalumu kwa ajili ya kuamsha ari ya wanachama wa TANU vilikuwa na athari
          kubwa, hasa wakati ambapo serikali ya kikoloni ilimpiga marufuku Mwalimu Nyerere

          kufanya mikutano ya hadhara.

          Ili kukwepa marufuku hiyo, TANU iliandaa hafla za taarabu na Mwalimu Nyerere
          alikuwa akikaribishwa kama mgeni rasmi. Mwalimu Nyerere alisimama kufungua
          hafla hizo na, kwa kufanya hivyo, alisema maneno machache kuhusu harakati za

          kudai uhuru. Kwa njia hii, ari ya kudai uhuru iliendelea kuwaka na Mwalimu Nyerere
          aliweza kuwasiliana na wananchi. Vilevile, kupitia taarabu, TANU ilikusanya fedha
          kwa ajili ya kuendeleza harakati za ukombozi.


                              Zoezi la         4.2


            1.  Je, ni kwa namna gani mbinu ya kuanzisha vyama vya kiraia ilisaidia
               harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar?
            2.  Jadili nafasi ya vyombo vya habari katika harakati za kisiasa wakati wa sasa.

            3.  Fafanua nafasi ya vijana katika kudumisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.

            4.  Eleza mchango wa vikundi na vyama vya kijamii na kidini katika kukukuza
               demokrasia wakati wa sasa.

            5.  Pendekeza mikakati ya kudumisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.








                                                  66




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   66                                         03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   66
   69   70   71   72   73   74   75   76   77   78   79