Page 79 - Historia_Maadili
P. 79

mazao na unafuu wa pembejeo za kilimo. Vyama mashuhuri vilikuwa ni pamoja na
          Kilimanjaro Native Cooperative Union (KNCU), Victoria Federation of Cooperative
          Union (VFCU), Bukoba Bahaya Union na Umoja wa Meru. Vyama hivi na vingine
          vilijenga mshikamano miongoni mwa wananchi na wakati wa harakati za kupigania
          uhuru, vilitoa mchango mkubwa wa kisiasa na hatimaye kuwa sehemu ya chama
          cha ukombozi cha Tanganyika African National Union (TANU). Hivyo, harakati
        FOR ONLINE READING ONLY
          za kupinga uvamizi wa wakoloni na kupigania uhuru zilichangia katika utunzaji wa
          maadili ya mshikamano ambayo yanaenziwa na taifa letu hadi sasa.

          Kiswahili
          Harakati za kupinga ukoloni na kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar zilitumia
          lugha ya Kiswahili kwa namna mbalimbali. Mathalani, Kiswahili kilitumika kusaidia
          kuleta umoja na mshikamano miongoni mwa wanachama wa TANU na ASP pamoja
          na wananchi wote. Lugha ya Kiswahili pia ilitumika kuwaunganisha wananchi wa
          Tanganyika na Zanzibar ili kupigania uhuru wa nchi zao. Wananchi wa nchi hizo,
          licha ya kwamba walitoka katika makabila na jamii tofauti, lugha ya Kiswahili
          iliwaunganisha na kuwafanya kuwa kitu kimoja katika kupigania nchi zao. Aidha,
          lugha ya Kiswahili ilisaidia kupeleka ujumbe kwa Watanganyika na Wazanzibari
          kwani ilitumika na wengi. Mbinu na mikakati iliyotolewa kuhusu uzalendo na ari
          ya kujitolea kupambana na ukoloni iliwasilishwa kwa kutumia lugha ya Kiswahili.
          Vilevile, katika harakati za kupambana na ukoloni, nyimbo, hasa taarabu, zilitumia
          lugha ya Kiswahili kupeleka ujumbe. Vyombo vya habari, kama vile magazeti ya
          Afrika Kwetu, Mkombozi, Mwiba, Sauti ya Afro-Shirazi, Ukombozi na Sauti ya
          Jogoo, vilitumia Kiswahili kuelimisha na kutoa habari kwa wananchi kuhusu harakati
          za kupigania uhuru.

          Aidha, sera na itikadi za TANU na ASP zilielezwa kwa lugha rahisi ya Kiswahili,
          hivyo kurahisisha ufikishaji wa ujumbe kwa wananchi. Viongozi waliamua kutumia
          lugha ya Kiswahili ili kueneza na kufikisha kwa urahisi sera za vyama vyao kwa
          wananchi. Wananchi walihamasishwa kutumia Kiswahili katika mawasiliano, jambo
          lililosaidia kuondoa hali ya ukabila na ubaguzi wakati wa kupigania uhuru. Kiswahili
          kilikuwa nguzo muhimu katika kufikisha taarifa na habari juu ya harakati za kupigania
          uhuru na kilisaidia kuwaunganisha wananchi hadi kufikia hatua ya kupatikana kwa
          uhuru wa Tanganyika na Zanzibar.


          Kujenga uzalendo
          Harakati za kupinga ukoloni zilihusisha kupinga sera na hata kuhusisha kupigana
          vita dhidi ya wakoloni. Katika harakati za kupinga ukoloni, Watanzania walionesha
          na kujenga uzalendo kwa jamii zao pale waliposimama kidete kuupinga uvamizi na

          utawala wa kikoloni kwa sera zao za unyonyaji na ukandamizaji. Pia, Watanzania
          walipinga kuingia kwa utawala wa kikoloni kwa kupambana kivita dhidi ya wavamizi


                                                  71




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   71                                         03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   71
   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84