Page 81 - Historia_Maadili
P. 81

ushiriki wao katika kuanzisha na kusimamia vyama vya siasa. Kupitia vyama hivyo,
          viongozi hawa walihamasisha uzalendo kwa kuwaongoza wanachama na hata
          wananchi kudai uhuru na haki zao. Mbali na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
          na Sheikh Abeid Amani Karume, kulikuwa na wazalendo wengine ambao nafasi
          yao kubwa ilikuwa kufadhili harakati za uhuru kwa hali na mali. Miongoni mwao
          walikuwemo John Rupia, Dossa Aziz, Abdulwahid Sykes na wengine. Uzalendo huu
        FOR ONLINE READING ONLY
          ulienea nchi nzima, ambapo watu walijitolea mali zao kusaidia harakati za uhuru.
          Kwa mfano, Aikael Mbowe (Kilimanjaro), Hamisi Heri na Sadiki Patwa (Tanga),
          pamoja na Suleiman Masudi Mnonji (Lindi).

          Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na viongozi wengine, waliongoza chama
          cha TANU kwa uzalendo hadi kufanikiwa kuikomboa Tanganyika kutoka kwa utawala
          wa kikoloni. Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alitembelea sehemu mbalimbali
          za Tanganyika katika juhudi za kuimarisha chama cha TANU. Kazi kubwa ilikuwa
          kuwaandaa wananchi kwa ajili ya madaraka na uhuru. Pia, TANUkwa kushirikiana
          na vyama vya wakulima na wafanyakazi, waliwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu
          wa kujiunga na TANU ili kufanikisha kumng’oa mkoloni.

          Hata hivyo, mwaka 1955, Julius K. Nyerere alitumwa na chama chake kwenda New
          York, makao makuu ya Umoja wa Mataifa, ili Umoja huo uwashawishi Waingereza
          kuipa Tanganyika uhuru wake. Mwaka 1957, Mwalimu Julius K. Nyerere aliteuliwa
          kujiunga na Baraza la Kutunga Sheria - Legislative Council (LEGCO).

          Haikuwa rahisi kwa TANU kusonga mbele bila vikwazo. Waingereza waliwakataza
          watumishi wa serikali kujiunga na vyama vya siasa. Pia, mikutano ya hadhara ilipigwa
          marufuku na matawi ya TANU yalifungwa katika baadhi ya maeneo kwa lengo la
          kuidhoofisha TANU. Hata hivyo,
          chama hiki kiliendelea kusonga
          mbele  na  kushinda  kwenye
          uchaguzi wa mwaka 1958/1959.
          Katika uchaguzi wa mwaka
          1960, TANU ilishinda na kupata
          wajumbe wengi katika Baraza
          la  Kutunga  Sheria. Ushindi  huo
          uliwaharakisha    Watanganyika
          kupata uhuru wao mapema. Uhuru
          ulipatikana tarehe 9 Desemba 1961.
          Kielelezo 4.9 kinaonesha picha ya   Kielelezo 4.9: Wananchi wakisherehekea uhuru wa
          wananchi wakisherehekea uhuru                 Tanganyika mwaka 1961
          wa Tanganyika.


                                                  73




                                                                                        03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   73                                         03/10/2024   18:15:16
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   73
   76   77   78   79   80   81   82   83   84   85   86