Page 86 - Historia_Maadili
P. 86

Kuanzishwa kwa sera ya  Afrikanaizesheni: Hii ni sera iliyowapa madaraka
          Watanganyika na Wazanzibari wazawa. Sera hii ililenga kutoa nafasi za uongozi na
          ajira kwa wazawa ambazo awali zilikuwa zikishikiliwa na Wazungu na Waasia wakati
          wa utawala wa kikoloni. Watanganyika na Wazanzibari wenye ujuzi walihamasishwa
          kufanya kazi serikalini na katika mashirika ya umma.

          Kuanzishwa kwa mifumo ya ulinzi na usalama: Ulinzi na usalama wa nchi ulikuwa
        FOR ONLINE READING ONLY
          ni suala lingine ambalo serikali iliweka mkazo katika kujenga taifa. Jitihada mbalimbali
          zilianzishwa ili kuhakikisha nchi inakuwa salama. Mfumo wa ulinzi na usalama wa
          taifa ulifayika kuanzia ngazi ya chini kupitia mfumo wa ubalozi wa nyumba kumi.
          Huu ulikuwa ni mfumo wa kiulinzi uliowezesha kujua ni nani anaingia na kufanya
          nini ndani ya nchi. Kwa kutumia mfumo huu, ilikuwa rahisi kuwabaini wageni na
          wahalifu hivyo, kuimarisha ulinzi na usalama katika makazi ya wananchi wote.
          Mfumo huu ulilenga kubaini shughuli, makazi na tabia za wananchi wote pamoja na
          wageni wao. Pia, kwa wale waliokuwa wakisafiri walipaswa kuripoti kwa balozi ili
          wajulikane walikotoka na wanakoelekea. Kila balozi alikuwa na jukumu la kusimamia
          eneo lake na kutatua changamoto husika au kuziwasilisha kwa mamlaka zinazohusika
          za serikali. Mfumo huu ulisaidia katika kulinda usalama, kujenga mshikamano,
          kusimamia mila na desturi za Kitanzania na kutatua changamoto mbalimbali za
          kijamii katika ngazi ya nyumba kumi.

          Ili  kuimarisha ulinzi na usalama,  Jeshi la
          Wananchi wa Tanzania (JWTZ) liliundwa
          mwaka 1964. Tanzania ilirithi jeshi la kikoloni
          lililojulikana kama  King’s  African  Rifles
          (KAR), ambapo nafasi nyingi za juu zilikuwa
          zikishikiliwa na wageni, yaani  Wazungu
          na Waasia. Mara baada ya uhuru, jeshi hili
          lilibadilishwa jina na kuitwa  Tanganyika
          Rifles (TR) hadi mwaka 1964 lilipoanzishwa
          JWTZ. Hii ni kufuatia maasi ya jeshi la TR
          mwaka 1964 na serikali kuamua kuwafukuza
          waasi wote kutokana na kukosa utii, uaminifu
          na uzalendo. Brigedia Mirisho Sam Hagai
          Sarakikya aliteuliwa kuwa mkuu wa majeshi      Kielelezo 5.2: Brigedia Mirisho Sam
          (Kielelezo 5.2).                                       Hagai Sarakikya

          Baada ya kuanzishwa kwa JWTZ, serikali ikawa makini kuteua na kuchagua watu
          waliounda jeshi jipya. Kwa sehemu kubwa, jeshi hili liliundwa na vijana watiifu,
          waadilifu na wazalendo kutoka Chama cha TANU na ASP. Hivyo, chini ya uongozi
          wa Brigedia Sarakikya waliunda Jeshi la nchi kavu (infantry), jeshi la majini (navy)
          na jeshi la anga (airforce). Pia Jeshi jipya lilianzisha shule za wapiganaji na vyuo
          vya maofisa.  Sarakikya aliongoza jeshi kuanzia 1964 hadi 1974.

                                                  78




                                                                                        03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   78                                         03/10/2024   18:15:17
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   78
   81   82   83   84   85   86   87   88   89   90   91