Page 91 - Historia_Maadili
P. 91

Cuban Marimba Band na Jamuhuri Jazz Band. Bendi hizi zilivutia mashabiki wengi
          kwa mtindo wa muziki wa rumba na cha-cha-cha. Mlimani Park Orchestra (Sikinde)
          ilianzishwa mwaka 1978, lakini chimbuko lake lilikuwa katika miaka ya 1960 na
          baadaye ikawa mojawapo ya bendi kubwa sana nchini. Kielelezo 5.3 kinaonesha
          baadhi ya waimbaji wa bendi ya muziki ya NUTA wakiwa jukwaani.

        FOR ONLINE READING ONLY



























                                     Kielelezo 5.3: NUTA Jazz Band


           Kazi ya kufanya 5.4


            Kwa kutumia mtandao au maktaba mtandao, soma matini mbalimbali na chunguza
            mchango wa lugha ya Kiswahili katika kujenga utambulisho wa taifa mara baada
            ya uhuru. Baada ya uchunguzi andika ripoti fupi kwa maneno yasiyozidi ukurasa
            mmoja.




                              Zoezi la          5.3


            1.  Je, ni kwa namna gani sanaa na muziki vinaweza kuendelea kutumika kama
               nyenzo za kuyajenga maadili na uzalendo katika Tanzania ya sasa?

            2.  Eleza nafasi ya sanaa katika kuleta maendeleo ya jamii.

            3.  Eleza nafasi ya Kiswahili katika kuuendeleza na kuudumisha utamaduni wa
               Mtanzania kwa  kizazi cha sasa.





                                                  83




                                                                                        03/10/2024   18:15:18
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   83
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   83                                         03/10/2024   18:15:18
   86   87   88   89   90   91   92   93   94   95   96