Page 94 - Historia_Maadili
P. 94

Kazi ya kufanya 5.5

            Tafuta taarifa kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo mtandao na andika maelezo
            zaidi kuhusu uanzishwaji wa mfumo wa chama kimoja cha siasa na mchango
        FOR ONLINE READING ONLY
            wake katika ujenzi wa taifa.




                              Zoezi la          5.4


            1.  Eleza mchango wa mfumo wa chama kimoja katika ujenzi wa taifa katika
               kipindi cha 1961 hadi 1966.

            2.  Ni kwa namna  gani  tatizo  la  ardhi  Zanzibar  lilitatuliwa  mara  baada  ya
               Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar?

            3.  Fafanua mchango wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) katika kukuza maadili na
               uzalendo kwa vijana mara baada ya uhuru.
            4.  Toa sababu tano zilizosababisha serikali kuvunja mamlaka za jadi mwaka
               1962.




          Changamoto za ujenzi wa taifa
          Kipindi cha mwaka 1961 hadi 1966 Taifa lilipitia changamoto mbalimbali za kiuchumi.
          kijamii na kisiasa. Kwa mfano, sekta ya kilimo ilipitia changamoto mbalimbali
          ikiwemo matumizi ya zana duni. Pia, kulikuwa na ukosefu wa wataalamu wa kilimo na
          uhaba wa masoko ya uhakika ya bidhaa. Hata hivyo, viwanda vilikuwa havijaimarika
          kutokana na upungufu wa wataalamu wa kuviendesha na pia kulikuwa na uhaba wa
          vipuri. Matatizo ya kifedha na mitaji yaliathiri juhudi za awali za kuleta maendeleo
          nchini. Aidha, kukosekana  kwa uhusiano wa moja kwa moja kati ya kilimo na
          viwanda kuliathiri maendeleo ya sekta zote mbili. Hata hivyo, pamoja na changamoto
          hizi zote, pato la taifa liliendelea kukua na kuimarika na hili liliendelea kuipa Tanzania
          heshima kimataifa. Kwa ujumla, kulikuwa na changamoto kadhaa zilizoathiri ujenzi
          wa taifa mara baada ya uhuru.

          Uasi wa jeshi mwaka 1964: Uasi wa Januari 20-27, 1964, pale Colito (sasa Lugalo),
          ambapo kikundi kidogo cha wanajeshi wa Tanganyika Rifles (TR) kiliasi na kutaka
          kuipindua serikali. Jaribio hilo lilizimwa na waliohusika walipewa adhabu kali, kama
          kufukuzwa jeshini, kufungwa na kuwekwa kizuizini kwa muda mrefu. Uasi huu
          ulisababisha kuundwa kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).



                                                  86




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   86
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   86                                         03/10/2024   18:15:19
   89   90   91   92   93   94   95   96   97   98   99