Page 98 - Historia_Maadili
P. 98

Aina ya pili ni mapinduzi ya kijeshi. Mapinduzi haya hufanywa na jeshi kwa lengo
          la kuondoa utawala uliopo madarakani kwa kutumia mapigano au mbinu za kijeshi.
          Mfano wa mapinduzi ya aina hii ni yale yaliyotokea Misri yakiongozwa na Kanali
          Gamal Abdel Nasser dhidi ya Mfalme Farouk I mwaka 1952, mapinduzi ya Mengistu
          Haile Mariam wa Ethiopia dhidi ya Haile Selassie mwaka 1974, mapinduzi ya Jenerali
          Iddi Amin Dada wa Uganda dhidi ya Rais Milton Obote mwaka 1971 na mapinduzi
        FOR ONLINE READING ONLY
          ya Libya chini ya Kanali Muammar Gaddafi dhidi ya Mfalme Idris mwaka 1969.



                              Zoezi la          6.1


            1.  Eleza sababu zilizosababisha Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

            2.  Fafanua namna uzalendo na ujasiri ulivyochangia kufanyika kwa Mapinduzi

               ya Zanzibar.
            3.  Jadili umuhimu wa kuyalinda Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.







           Kazi ya kufanya 6.1

            Umeteuliwa kushiriki katika mdahalo wenye mada isemayo “Mapinduzi ilikuwa
            ndio njia pekee ya Wazanzibari kujikwamua kutoka katika ukoloni.” Soma vitabu
            na matini mbalimbali kisha andaa dondoo utakazotumia wakati wa mdahalo.




          Chimbuko la Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
          Zanzibar ilikuwa chini ya utawala wa kisultani hadi mwaka 1890. Kama ilivyotajwa
          awali, Sultani Seyyid Saidi alikuwa sultani wa kwanza kuongoza dola mbili, yaani
          Oman na Zanzibar, akiifanya Zanzibar kuwa makao makuu ya himaya hizo. Sultani
          Seyyid Said alihamia Zanzibar mwaka 1840 akitokea Muscat, Oman. Mnamo mwaka
          1890, Zanzibar iliwekwa chini ya utawala wa Waingereza na ikatambulika kama
          Mahamia ya Uingereza au “British Protectorate.” Katika hali hiyo, utawala wa sultani
          ulitumiwa na Waingereza katika kuitawala Zanzibar. Hali hii ilisababisha mgawanyiko
          mkubwa kati ya Waarabu wachache, ambao walikuwa na nguvu kubwa za kisiasa
          na kiuchumi na Waafrika walio wengi ambao hawakuwa na nguvu zozote zaidi ya
          umasikini na kutumikishwa na Waarabu pamoja na wageni wengine wakiwemo
          Waingereza na Waasia.




                                                  90




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   90
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   90                                         03/10/2024   18:15:19
   93   94   95   96   97   98   99   100   101   102   103