Page 48 - Historia_Maadili
P. 48

ya Majimaji, iliyopiganwa kuanzia mwaka 1905 hadi 1907. Vilevile, nyimbo hizi
          zilitumika kuwahamasisha na kuwaunganisha wapiganaji dhidi ya majeshi ya kikoloni
          ya Wajerumani.

          Kadhalika, utamaduni wa masimulizi ulisaidia kueneza elimu kwa vizazi vichanga
          kuhusu maadili, kanuni za kijamii na stadi maisha. Wakati wa ukoloni, mifumo
        FOR ONLINE READING ONLY
          rasmi ya elimu ilidhibitiwa na wakoloni, hivyo jamii zilihakikisha kwamba watoto
          wa Kitanzania wanaendelea kujifunza utamaduni na historia yao kupitia kwa wazee.
          Kwa mfano, miongoni mwa jamii za Wanyamwezi, wazee walisimulia hadithi ili
          kutoa mafunzo kuhusu ushujaa, hekima na umuhimu wa jumuiya, ambayo yalikuwa
          muhimu katika kusaidia jamii kukabiliana na changamoto za utawala wa kikoloni.


                              Zoezi la           2.5


            1.  Kwa nini wakoloni walishindwa kutokomeza maadili ya Kitanzania pamoja
               na jitihada kubwa walizozifanya?

            2.  Eleza umuhimu wa masimulizi katika kuyadumisha maadili ya Kitanzania.
            3.  Bainisha  maadili  mengine  ya  jamii  za  Kitanzania  yaliyodumu  licha  ya
               ushawishi wa utawala wa kikoloni kuyafuta.

            4.  Eleza mchango wa serikali ya Tanzania katika kuenzi na kudumisha maadili
               ya Kitanzania.



          Mavazi: Jamii za Kitanzania ziliendelea kuenzi mavazi yao ya kiasili hata katika
          kipindi cha ukoloni.  Jamii mbalimbali zilichukua juhudi za kipekee kuendeleza na
          kusambaza maarifa ya mavazi ya jadi kwa vizazi vilivyofuata, zikitambua umuhimu
          wa kuheshimu na kudumisha utamaduni wao wa kipekee licha ya shinikizo kubwa la
          kuvaa mavazi tofauti yaliyoletwa na wageni. Mavazi ya Ulaya Magharibi yalijenga
          taswira ya ubora wa utamaduni wao, imani mpya, nguvu, ustaarabu na usomi. Mavazi
          ya asili yalienziwa kupitia matamasha, mikusanyiko na sherehe mbalimbali za kijadi

          kama vile sherehe za mavuno, jando na unyago, harusi na tohara.



           Kazi ya kufanya 2.5


            Fanya utafiti katika jamii unamoishi na bainisha maadili ya jamii za Kitanzania
            yaliyokuwepo wakati wa ukoloni ambayo bado yanaenziwa hadi wakati wa sasa.






                                                  40




                                                                                        03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   40
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   40                                         03/10/2024   18:15:11
   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53