Page 43 - Historia_Maadili
P. 43

Mavazi: Baada ya ujio wa ukoloni, kulianza kujitokeza mabadiliko ya taratibu katika
          mitindo ya mavazi. Mavazi ya Kimagharibi kama vile suti, tai, magauni, kaptula,
          suruali na mengineyo, yalianza kuingizwa na kukubalika, hasa miongoni mwa
          walioelimika au wale waliokuwa na ushawishi katika utawala wa kikoloni. Hii
          ilisababisha kudunishwa au kupuuzwa kwa mavazi na maadili ya kijadi ya mavazi.
          Mabadiliko haya mara nyingi yalisababisha kuachwa
        FOR ONLINE READING ONLY
          kwa  mavazi  ya  kiutamaduni,  kwani  mitindo  ya
          Kimagharibi ilihusishwa na usasa, maendeleo, ustaarabu,
          nguvu za utawala na heshima. Pia, maadili na tabia za
          jamii zilianza kubadilika kutokana na ushawishi wa
          utamaduni wa kigeni wa mavazi.
          Vilevile, katika maeneo ya pwani, hasa miongoni
          mwa jamii za Waswahili, mavazi yaliathiriwa sana
          na utamaduni wa Kiarabu kutokana na karne nyingi
          za biashara na mwingiliano. Kwa kawaida, wanaume
          wa Kiarabu huvaa “kanzu,” vazi refu ambalo mara
          nyingi huwa na rangi nyeupe, huku wanawake wakivaa
          “baibui” vazi jeusi linalofunika mwili mzima. Mavazi
          ya Waswahili kwa kiasi kikubwa yaliakisi utamaduni
          wa Kiarabu. Vielelezo 2.3 na 2.4 vinaonesha baadhi ya   Kielelezo 2.3: Vazi la baibui
          mavazi yaliyoletwa  na wageni.

































                                   Kielelezo 2.4:  Vazi la suti na kanzu



                                                  35




                                                                                        03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   35                                         03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   35
   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48