Page 47 - Historia_Maadili
P. 47

Ukarimu:  Jamii za Kitanzania zilijulikana kwa ukarimu wao na  thamani hii
          iliendelezwa hata wakati wa ukoloni. Jamii hizi ziliamini katika umuhimu wa
          kuwatendea wageni kwa heshima na ukarimu. Pia, jamii hizi ziliendelea kusisitizwa
          kuonesha uvumilivu na utu katika kuishi na kushirikiana na watu wa tamaduni
          tofauti, huku wakijifunza na kuchangamana nao. Thamani ya umoja na mshikamano
          ilisisitizwa katika kukabiliana na changamoto za ukoloni, kihistoria na kiuchumi,
        FOR ONLINE READING ONLY
          ambapo jamii hizi zilipigania uhuru na haki ya kujitawala.

          Utii kwa mamlaka: Wakati wa utawala wa kikoloni, heshima kwa uongozi wa ndani
          na miundo ya kimila iliendelea kudumishwa. Heshima hii ilienea pia kwa watawala wa
          kikoloni, ingawa mara nyingi iliambatana na upinzani. Kwa mfano, chini ya utawala
          wa kikoloni, jamii nyingi za Kitanzania ziliendelea kuwaheshimu viongozi wao wa
          kimila kama machifu, wazee na wakuu wa koo. Viongozi hawa walionekana kama
          mamlaka halali zinazosimamia masilahi ya jamii. Kwa mfano, jamii za Wachaga na
          Wahehe ziliendelea kuwaheshimu machifu wao, ambao walijulikana kama Mangi
          na Mtwa mtawalia, kama viongozi wao halali. Licha ya kuwepo kwa watawala wa
          kikoloni, jamii nyingi za Kitanzania mara nyingi zilishauriana na machifu wao katika
          kutoa uamuzi na miongozo mbalimbali. Hali ambayo ilidhihirisha heshima kwa
          mifumo yao ya utawala wa kimila.

          Utamaduni wa masimulizi: Uwasilishaji wa historia, utamaduni na maadili kupitia
          masimulizi, hadithi, mashairi, methali na nyimbo ulibaki kuwa njia muhimu ya
          kuhifadhi historia na utambulisho wa makabila/jamii mbalimbali za Kitanzania.

          Maadili haya yalikuwa muhimu kwa mifumo ya jamii za Kitanzania. Hii ilisaidia
          kudumisha utambulisho na mwendelezo hata chini ya utawala wa kikoloni. Simulizi
          hizi zilikuwa na mchango mkubwa katika kuhifadhi historia, maadili na imani za
          jamii za Kitanzania na zilizuia rekodi hizi kupotoshwa na wakoloni.

          Vilevile, mapokeo ya simulizi yaliwezesha jamii kudumisha utambulisho wao kwa
          kurithisha hadithi, methali, nyimbo, utani na ngano ambazo zilikuwa na urithi wao
          wa kitamaduni. Kwa mfano, hadithi kuu za Wasukuma, ambazo zilirithishwa kutoka
          kizazi kimoja hadi kingine, zilibeba kumbukumbu ya hekima na ujasiri wa mababu zao
          na zilitumika kama chanzo cha fahari na utambulisho, hata wakati ambapo wakoloni
          walijaribu kukandamiza tamaduni za wenyeji.

          Aidha, utamaduni wa masimulizi ulichangia kueneza hisia za kupinga ukoloni. Kwa
          mfano, hadithi na nyimbo zilitumika kukosoa mamlaka za kikoloni, kutia moyo
          ujasiri na kukuza mshikamano miongoni mwa wanyonge. Mathalani, nyimbo na
          ngoma miongoni mwa jamii za Wangoni waliopo kusini mwa Tanzania zilijumuisha
          ujumbe wa upinzani dhidi ya majeshi ya kikoloni ya Wajerumani wakati wa Vita


                                                  39




                                                                                        03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   39                                         03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   39
   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52