Page 46 - Historia_Maadili
P. 46

Ingawa kulikuwa na jitihada kadhaa za kubadilisha maadili hayo kutokana na
          ushawishi wa wakoloni, bado maadili yaliendelea kuwa nguzo muhimu katika jamii.
          Katika awamu ya mwisho ya ukoloni, mawazo ya utaifa na harakati za uhuru yaliibuka
          na kuungwa mkono na baadhi ya wazungu wenye msimamo huria. Hali hii ilichangia
          kuunda maadili mapya ya kisiasa na kijamii, ambapo watu walihimizwa kujivunia
          utambulisho wao wa Kitanzania na kupinga utawala wa kikoloni. Hata hivyo, wakati
        FOR ONLINE READING ONLY
          wa ukoloni, baadhi ya maadili ya kiutamaduni ya Kitanzania yaliendelea kuhifadhiwa
          na jamii za wenyeji. Baadhi ya maadili haya yanaelezwa katika sehemu zinazofuata.

          Umoja na ushirikiano: Dhana ya maisha ya jumuiya na uwajibikaji wa pamoja
          ilikuwa tunu kuu katika jamii nyingi za Kitanzania. Kwa mfano, miongoni mwa
          Wachaga wa Kilimanjaro, kilimo cha jumuiya na kazi za pamoja zilikuwa na umuhimu
          mkubwa. Vitendo hivi vilichangia kudumisha mshikamano wa kijamii na kuhakikisha
          kwamba hakuna mwanajamii aliyeachwa nyuma, hata katika mazingira ya shinikizo
          la utawala wa kikoloni. Shughuli za pamoja kama vile kilimo, ujenzi, au shughuli
          nyingine za kijamii zilifanywa kwa manufaa ya jamii nzima ili kuimarisha uhusiano
          wa kijamii.

          Heshima kwa wazee: Licha ya utawala wa kikoloni, jamii za Kitanzania ziliendelea
          kuzingatia kanuni za kiutamaduni zilizosisitiza heshima kwa wazee. Kwa mfano,
          jamii za Wazaramo wa eneo la pwani ziliendelea kushikilia maadili haya wakati wa
          ukoloni, ambapo wazee walitumika kutoa ushauri na kufanya uamuzi. Aidha, wazee
          walikuwa walinzi wa maarifa, mila, ujuzi na mapokeo ya kijamii.

          Vilevile, jamii ya Wamasai iliendelea kushikilia tamaduni zao za kuonesha heshima
          kwa wazee na viongozi wa jadi. Heshima hii kwa viongozi ilikuwa muhimu kwani
          ilidumisha umoja na mshikamano wa kijamii. Hivyo,  kudumisha utulivu wa kijamii na

          mwendelezo wa utamaduni na maadili, licha ya usumbufu uliosababishwa na ukoloni.
          Kwa ujumla, kuheshimu wazee na watu waliowazidi umri kulikuwa na nafasi kubwa
          katika jamii nyingi za Kitanzania hata katika kipindi cha ukoloni.

          Mifumo ya haki ya jadi: Jamii nyingi za Kitanzania ziliendelea kutumia mifumo
          yao ya haki ya jadi katika kutatua migogoro. Kwa mfano, miongoni mwa jamii za
          Wasukuma katika Kanda ya Ziwa, kulikuwa na mabaraza ya kimila yaliyowajibika
          kusuluhisha migogoro ndani ya jamii. Mabaraza haya, yalishirikiana na mfumo
          wa kisheria wa kikoloni lakini yalisalia kuwa chombo muhimu cha kudumisha
          sheria na utulivu ndani ya jamii. Jambo hili linadhihirisha  uimara wa mifumo ya
          utawala wa kimila. Mifano hii inaonesha jinsi tunu za Kitanzania zilivyohifadhiwa
          na kubadilishwa wakati wa ukoloni na hivyo kuonesha uthabiti wa mila na desturi
          katika kukabiliana na athari za nje.


                                                  38




                                                                                        03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   38                                         03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   38
   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51