Page 42 - Historia_Maadili
P. 42

ustaarabu ulianza kupimwa kwa kujua lugha za kigeni na utamaduni wa kikoloni
          kama lugha, mavazi, aina ya vyakula na kazi za ofisini na utawala.

          Aidha, ukoloni ulisababisha kutengenezwa kwa vitabu na nyaraka nyingi kwa lugha
          za kikoloni badala ya lugha za asili, hivyo kusababisha upungufu wa vyanzo vya
          maarifa kwa lugha za asili za Tanzania. Hii ilisababisha watoto kujifunza masomo
        FOR ONLINE READING ONLY
          yao yote kwa lugha za kigeni na hivyo kupoteza uwezo wao wa kujieleza vizuri

          kwa lugha zao za asili. Kama inavyoaminika na wataalamu wengi wa elimu, hali hii
          iliwafanya wanafunzi wapoteze uwezo wao wa ubunifu, kuelewa na kujiamini, kwa
          sababu lugha waliyoitumia haikuwa ya asili yao. Hata hivyo, kwa Tanzania, ukoloni
          ulitumia lugha ya Kiswahili kwa shughuli za Waafrika kama kutoa maelekezo na
          kendesha kesi katika mahakama za wenyeji zilizosimamiwa na machifu.

          Zaidi ya hayo, mifumo ya elimu ya kikoloni ilisababisha kuibuka kwa msamiati
          wa kigeni. Kwa mfano, maneno mengi ya Kiingereza na Kijerumani yalipokelewa,
          kutoholewa na kutumika katika Kiswahili. Mfano wa maneno haya ni “shule” kutoka

          “schule,” “nanasi” kutoka “ananas,” na “hela” kutoka “heller” yalitoka katika
          lugha ya Kijerumani. Pia, maneno kama “polisi” kutoka “police,” “benki” kutoka
          “bank,” “baiskeli” kutoka “bicycle,” na “hospitali” kutoka “hospital” yalitoka katika
          lugha ya Kiingereza. Vilevile, athari za lugha za kikoloni zimejidhihirisha kupitia
          maneno, misemo na mabadiliko ya sarufi. Mabadiliko haya yanaonesha jinsi ukoloni
          ulivyoweza kubadilisha matumizi ya lugha za Kitanzania na kuathiri utamaduni na
          mawasiliano ya kila siku.


          Katika kipindi cha 1890-1961, Kiswahili kiliathiriwa sana na kuingiliana na lugha za
          kikoloni. Ushawishi wa kikoloni, kama vile Wajerumani, ambao walikuwa wakoloni
          wa kwanza nchini ulijidhihirisha kupitia matumizi ya lugha ya Kijerumani kwenye
          baadhi ya masuala ya utawala na kidogo sana kwenye elimu. Baadaye, Waingereza
          walipochukua mamlaka baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Kiingereza kilitumika
          kama lugha ya kufundishia  shuleni na lugha rasmi ya serikali.



           Kazi ya kufanya 2.4


            Andika insha isiyopungua maneno 200 ukionesha:
             (a)  Umuhimu  wa kuhifadhi  na  kuendeleza  lugha  za  asili  kwa jamii  za
                  Kitanzania; na
             (b)  Mikakati ya kuhifadhi na kuendeleza lugha za asili kwa kizazi cha sasa
                  na kijacho.


                                                  34




                                                                                        03/10/2024   18:15:11
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   34
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   34                                         03/10/2024   18:15:11
   37   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47