Page 40 - Historia_Maadili
P. 40

magonjwa. Vilevile, huduma za afya za jadi zilihusishwa na imani za jadi, ambapo
          matambiko yalifanyika kutibu baadhi ya magonjwa.

          Ujio wa wakoloni ulileta mabadiliko makubwa katika mfumo wa afya, kwani
          walianzisha hospitali na vituo vya afya katika maeneo mbalimbali nchini kwa kutumia
          mtindo na mfumo wa Ulaya magharibi. Walileta pia dawa mbalimbali za kutibu
        FOR ONLINE READING ONLY
          magonjwa ambazo zilikuwa tofauti na zile za asili zilizotumika kabla ya ukoloni.

          Aidha, wakoloni walibeza na kudunisha  mfumo wa tiba za asili kwa kutumia mbinu
          mbalimbali kama vile dini, kugawa dawa za kimagharibi kwa jamii za Kitanzania na
          kueneza propaganda kuwa tiba za asili hazina msaada wowote, ni uchawi na ushirikina
          na ni alama ya umasikini na ukosefu wa maendeleo. Zaidi ya hayo, serikali ya kikoloni
          ilizuia na kuwakamata wataalamu wa tiba za asili, hatua ambayo iliathiri kwa kiasi
          kikubwa imani na maadili ya mfumo wa afya wa jadi. Ukweli unabaki kuwa dawa za
          Ulaya magharibi pia zilitokana na mimea na wanyama kama za Waafrika ila wazungu

          walizichakata viwandani, kuzifungasha katika vifungashio na waliziwekea vipimo
          maalumu ili kutibu ugonjwa unaohusika.


          Athari za kiutamaduni
          Ujio wa wakoloni ulileta athari mbalimbali za kiutamaduni kwa jamii za Kitanzania
          kama inavyoelezewa hapa chini.

          Dini za jadi: Kabla ya kuja kwa dini za kigeni kama Ukristo na Uislamu, jamii
          za Kitanzania zilikuwa na imani za kiasili zilizokita mizizi katika utamaduni wa
          jamii iliyohusika. Dini hizi mara nyingi zilihusisha ibada za kuabudu Mungu kupitia
          miungu, mababu na mizimu katika maeneo mbalimbali kama vile mapango, mito,
          mabwawa, milima, majabali makubwa na miti mikubwa. Imani za dini za jadi zilijikita
          katika kulinda na kudumusha maadili mema ya jamii.

          Ujio wa ukoloni nchini uliathiri na kuleta mifumo mipya ya imani na dini, ambayo
          iliendana na utamaduni wa Ulaya Magharibi. Kwa mfano, wamisionari wa Kikristo
          walileta mafundisho mapya yenye mila, desturi na maadili mapya, huku wakilenga
          kubadilisha imani za jamii za Kitanzania.  Aidha, dini za jadi za Kitanzania
          zilidharauliwa na kupigwa vita na wakoloni kama sehemu ya juhudi zao za kueneza
          mila na desturi za nchi za Ulaya Magharibi. Hii ilisababisha jamii nyingi za Kitanzania
          kuukubali mfumo wa dini za Kikristo na hivyo kuwa na maadili ya Ulaya Magharibi
          au maadili mseto. Maadili ya asili yalishambuliwa kuwa si bora, yaliwakandamiza,
          kuwabagua na kuwadunisha wanawake. Hivyo maadili ya asili yalipata mtikisiko
          mkubwa kutoka kwenye imani hii mpya ya Kikristo.

          Kwa ujumla, imani za asili zilichukua sura mpya, zikichanganywa na mafundisho ya
          Kikristo na utamaduni wa wakoloni. Matokeo yake, dini ya Kikristo ilipata msukumo

                                                  32




                                                                                        03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   32                                         03/10/2024   18:15:10
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   32
   35   36   37   38   39   40   41   42   43   44   45